Unateseka ukiwa wapi kijana? Hivi tangu jana umekunywa hata maji kweli? Maana najua usingizi hukupata sababu ya kutokuamini kile ulichokiamini pale Emirate.
Labda nikujuze tu wewe na wenzako mnaoishi kimazoea, Arsenal hii ya Sasa ina uwezo wa kucheza kwenye uwanja wowote dhidi ya mkubwa yoyote na ikapata matokeo, maana tayari wachezaji wa waliopo wana ile charisma ya kucheza mechi kubwa zenye pressure.
kwa mtu yeyote anayejua mpira yale matokeo ya jana hayawezi kumshangaza, maana katika ya timu zote 8 zilizobaki real madrid ni timu iliyofika hapa kwa uzoefu tu na na wala si kwa ubora.
Na ilikuwa ni suala la muda tu wakutane na timu iliyobora kuliko wao ya kuwa expose Kuwa wao ni timu dhaifu... angalia hata huko nyuma alipotoka amekutana na mbovu mwenzie manchester city na kibonde wake wa miaka yote Atletico madrid.
Jana tumeona gap kubwa sana la ubora kati ya gunners na madrid, halafu eti unategemea madrid ataenda kupindua ubao kwake bernabeu? Hizo ni ndoto za alinacha... Achana na habari za Liverpool vs barca.... ile liverpool haikuwa chujio hivi kama hii madrid ya sasa, na pia Arsenal haina defense mbovu kama ile barca ya 2019.
Labda kwa ushauri tu ukiwa kama muombea mabaya, hizo dua zako labda uziamishie kwa Inter ambaye tutakutana nae fainali, maana hapo nusu fainali sioni wa kutuzuia na pia kule upande wa pili sioni wa kumzuia Inter asifike fainali.