Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arteta ni kama anafanya majaribio na kikosi kwa hizi mechi mbili.. Ni kama hana uhakika na anachofanya. Una wachezaji ambao wanaweza kucheza beki wa pembeni vizuri unawaweka nje then mchezaji wako bora kabisa kwenye eneo la katikati unamchezesha out of position.
 
Tunakosa sana nafasi za wazi kiasi kwamba unaanza kuhisi tuna nafasi ndogo ya kusonga tukikutana na Elite teams kwenye hatua ya mtoano... Kwasababu haziwezi kukupa nafasi nyingi hivyo. Nafasi chache utakazopata inabidi uzitumie.
 
Kuna vitu Jesus anakupa Kai Havertz hawezi kukupa kamwe.. Kuna vitu Kai Havertz anakupa Jesus hawezi kukupa kwa sasa na amepoteza uwezo huo hasa anapokuwa 1vs1 na kipa. Hatuwezi kwenda mbele na aina hii ya wachezaji ambao wanabeba roho ya timu pale mbele. Arsenal wanamuhitaji namba tisa Kariba ya Alexander Isak.
 
Back
Top Bottom