Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Huyu Ramsdale sidhani kama ana akili timamu
Kipa wako mwenye akili uyu apa
IMG_20241005_201224.jpg
 
Ramsdale ni moja ya matahira hapa duniani
We jamaa huwa huna kazi ya kufanya aisee🤠🤠🤠...kabisa unakaa kuwategemea Southampton watuvue nguo sisi kwli???....wale hata tukicheza mechi siku 2 mfululizo halafu siku ya tatu tukacheza nao tena tunawafunga kirahisi tu....
 
Nikasema Wolves wapo kwenye form mbaya nikaambiwa wameanza na mechi ngumu.

Lets keep going

Ambacho hamuoni ni kwamba wanaanzia walipoishia. Walimaliza msimu hovyo, wameanza hovyo.

Mechi 17 wamepata points 6
 
Nikasema Wolves wapo kwenye form mbaya nikaambiwa wameanza na mechi ngumu.

Lets keep going

Ambacho hamuoni ni kwamba wanaanzia walipoishia. Walimaliza msimu hovyo, wameanza hovyo.

Mechi 17 wamepata points 6
Sasa nakubali mkuu, hii ni pattern kabisa

Lopetegui anazamisha mtumbwi
 
Kumbukumbu EPL 22/23 match week 7 Arsenal vs Bournemouth, ndani ya banda umiza.

Tunapata penalty, Odegard anampa ball Kai apige. Mashabiki wanagawanyika ndani ya banda umiza. Wengi wakisema anakosa huyo.

Mashabiki ya KENGE yanasikika yakisema, hakuna mpigaji wenu wa penalty anayemfikia HAVERTZ hapo Emirates. Kai anachukua ball, anaweka waah. Kai, aibu imemjaa hata kwenye kushangilia.

Msimu huu match week 7, banda umiza, baada ya first half, kila shabiki anataka second half Jesus apumzike, Kai awe CF. Dk ya 58 anaturudisha mchezoni!

Kai Lucas Havertz, kutoka katika goli la huruma, kuja kuwa mchezaji wa pili kufunga magoli 7 mfululizo ndani ya Emirates

premierleague-20241006-0001.jpg
20241005_213330.jpg
 
Ukweli ni kwamba ninyi sio wazuri sana ila mna upepo tu misimu hii miwili.
Mmepelekwa na SOTON kiasi kwamba isingekuwa bahati ilikuwa iwe ama draw au mfungwe kabisa.

Timu imepigwa na Man Utd mbovu goli 3 na clean sheet juu imewatoa jasho hivi halafu bado mnawaza ubingwa!
 
Zimekuwa za tabu sana kama City.
Hivi unafahamu pamoja na ubora wa Arsenal na ubovu wa difensi ya Man Utd kama mnavyotuzingua, bado tuna asilimia kubwa ya cleansheet kuliko ngome ya Saliba na Gaby na pazia lenu Raya?
 
Ukweli ni kwamba ninyi sio wazuri sana ila mna upepo tu misimu hii miwili.
Mmepelekwa na SOTON kiasi kwamba isingekuwa bahati ilikuwa iwe ama draw au mfungwe kabisa.

Timu imepigwa na Man Utd mbovu goli 3 na clean sheet juu imewatoa jasho hivi halafu bado mnawaza ubingwa!

Hivi unafahamu pamoja na ubora wa Arsenal na ubovu wa difensi ya Man Utd kama mnavyotuzingua, bado tuna asilimia kubwa ya cleansheet kuliko ngome ya Saliba na Gaby na pazia lenu Raya?
Rudi uendelee kulala.nahisi umekatisha usingizi wako mkuu
Yani kwa zile beki zenu, na huyo onana mchomeshaji ila bado unaifananisha na ukuta wa Arsenal
Maajabu hayajawahi isha duniani
 
Rudi uendelee kulala.nahisi umekatisha usingizi wako mkuu
Yani kwa zile beki zenu, na huyo onana mchomeshaji ila bado unaifananisha na ukuta wa Arsenal
Maajabu hayajawahi isha duniani
Namba hazidanganyi mkuu.
Onana clean sheet 3 ndani ya game 6 ni sawa na 50% ya mechi alizocheza
Saliba/Gaby na Raya clean sheet 3 ndani ya game 7 ni sawa na 42,7% ya mechi walizocheza.

Au wewe mkuu ubora wao unaupima kwa kigezo gani?
 
Back
Top Bottom