mkorea
JF-Expert Member
- Aug 16, 2016
- 7,408
- 16,332
Wakikuelewa nidai $50 cashKwa hiyo katika hiyo miaka 21, yote Arsenal imekuwa ikimilikiwa na Kroenke?
Na kabla ya hapo Arsenal ilikuwa haijahama kutoka kwenye stadium moja hadi ingine kwa kutumia pesa zake yenyewe na si za mfadhili mmoja?
Kipindi hicho Arsenal imekuwa haina deni la kulipa la hiyo stadium na ukiacha ubingwa tu, haikuwa ikitegemea top 4 qualification ili ipate pesa ya kulipa deni na kujiendesha?
Ni kweli kuna makosa mengi sana Arsenal ilifanya katika jitihada zake za upambanaji, mfano kupiga dili za sponsorship za hela ndogo ukilinganisha na wenzake kama kina Man Utd, scouting ya wachezaji bora, viongozi wahuni, nk. Matokeo ya makosa hayo yalionekana kwa Arsenal kushuka mpaka kuanza kukosa kabisa champions league.
Ila je huoni kwamba baada ya Wenger kuondoka Arsenal imefanya juhudi za dhati za kurejea juu? Huoni kwamba sasa kwa misimu miwili mfululizo tumegombania kombe? Huoni kwamba kwa misimi 4 au mitano sasa tumetoka kwenye kumaliza kwenye nafasi ya hovyo mpaka bora huku tukiongeza points msimu hadi msimu?
Ukisema 'hakuna kitu ndani ya miaka 21', sielewi wewe unatazamaje mafanikio ama progress. Mwaka huu tumefika points nyingi zaidi tulizowahi kushika na bado hatujashinda ligi. Hiyo si progress? Mwaka huu Kipara kashinda ligi na points 91, nadhani kuna mwaka ameshinda na points 101. Points 10 chini zaidi. Je hiyo ni progress?
Najua mambo mengine ni ushabiki tu na tunapenda sana yawe hivyo, ila watu wanabidi wachunge sana attitude za mafanikio kwa maono yako wasiyapeleke kwenye maisha yao maana mtu unaweza kushindwa kujua wapi unasonga na wapi unarudi nyuma.
Enzi za shule niliwahi kuongoza darasa na average ya 76%. Nyumbani full shangwe ila mimi niliuchuna sikusherekea. Sababu ilikuwa ni muhula uliopita nilikuwa na average ya 86% ila nilikuwa wa nne (niliingia top 4 ila bingwa alikuwa mwingine). Enzi hizo pass mark yangu binafsi ni 80, bila kujali wanafunzi wengine wamefaulu vipi, nikipata chini ya hapo naona nimefeli. Nikipata hapo na zaidi naona nimeelewa material.
Arteta na Arsenal nawaangalia kwa jicho la hivyo pia. Naponda sana ila pia naona tofauti kutoka tulipoporomoka mazima na sasa naona tumepanda na tunapanda.
Mnatuita false hopers kwa sababu tunataka ubingwa? Sasa kwani ni nini tunapambania? Si ubingwa? Hamtaki tuseme kuwa tunautaka huo ubingwa? Mnafikiri tunatosheka na top 4 siku hizi?