Hakika mkuu, siku hizi hautaji tu kuwa bora hili uweze kuchukua ligi, bali yakupasa uwe na ubora ambao hauna makosa kabisa... yaani kama unafanya mistakes basi hakikisha wapinzani wako nao wawe wamefanya mistakes ambazo zina impacts sawa na kwako.Ila kwa sasa guys ligi imebadilika saaana.
Mechi moja unayopoteza August inaweza ikakuhukumu may
Ni kama kocha na wachezaji wanatakiwa kuwa full perfect with no room for errors and correction
Ukitazama quality ya makocha walioko epl kwa sasa unauona ugumu wa kubeba ligi
Zamani ilikuwa ukishinda mechi 25 tu kati ya mechi 38 basi wewe moja moja kwa moja una uhakika wa ubingwa, Manchester united amechukua ubingwa mara 20, na mara zote hizo hakuwahi kushinda mechi zaidi ya 26, hata points nyingi alizowahi kuzifikisha ni 85, lakini ndio timu yenye mafanikio zaidi kwenye EPL, sababu ilikuwa ni bora tu.
Msimu wa 2018/2019 Liverpool alishinda mechi 31 na alimaliza na points 97 lakini bado akaukosa ubingwa..... hii inaonesha ni jinsi gani unaweza ukawa bora lakini bado ukakosa ubingwa kwa sababu hauna perfection.
Jana Arsenal tumeshinda mechi ya 26 tangu msimu umeanza na hizi ndio mechi nyingi tulizowahi kushinda tangu tupande daraja, kwa mara ya mwisho kushinda mechi nyingi hivi ilikuwa ni msimu wa 2003/2004(invincible season) ambapo tulishinda mechi 25.
Unaweza ukaona kipara ameweka standards za hali ya juu mno hili kuchukua ubingwa, yaani unahitaji karibu kila timu uwe unajipigia tu na hasa round ya pili.
Kwakweli ni kazi sana, ila ninachojivunia kuna mabadiliko makubwa sana kulinganisha na misimu mingi iliyopita huko nyuma. Acha tuone kesho Spurs pengine labda anaweza akatupa ubingwa licha ya chuki kali aliyonayo dhidi yetu