Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Nakubaliana na wewe hapa kwa namna ya mechi tulizopoteza. Ukitaka ubingwa wa ligi, hupaswi kufungwa zaidi ya mechi 3. Na pia hupaswi kutoka sare zaidi ya mechi 3 kwenye ligi yenye Man City ya Guardiola. Yule jamaa ni bonge la mmafia.

Ila kwenye kujifunza, sema tumejitahidi sana pia na kuna kihatua tumepiga. Pamoja na ujinga wa kutoshoot, tumeongeza idadi ya magoli ya kugunga. Kipa wetu kabeba golden glove. Wachezaji wetu wakiangalia msimu huu, watahuzunika kiasi kwa kupoteza ubingwa ila si kama msimu uliopita.

Arteta alianza na kumaliza wa 8 msimu miwili. Akaja kumaliza wa 5. Sasa anaweza kumaliza wa 2 misimu miwili mfululizo. Karika kumaliza wa 2, msimu mmoja aliachwa nyuma points 5, mwingine, huu, anaweza kuachwa kwa points 2.

Arteta ana mambo ya kijinga ila anajitahidi kujifunza na kuimarika mechi hadi mechi na msimu hadi msimu. Wachambuzi kadhaa wanasema hili suala la kujifunza (kwa haraka) ni moja kati ya silaha zake kubwa zinazomtenga yeye na makocha wengine.
Pia tumejitahidi kuwafunga washindani wetu wakiwemo Man City.
 
Shekhee Hamis amepotea wapi? Yeye ndo mchambuzi wa uhakika ila akifungwa anakimbia jukwaa....hana kifua. Kabisa.
 
Umemsahau Pep ni shetani wa aina gani?
Sisi tunatakiwa u kujitahidi kushinda mechi zetu ili tujihakikishie kwamaba tumepiga hatua, kwamba msimu huu ni bora kuliko iliyopita. Ila ubingwa ni kitu kisichowezekana katika hali hii.
Spurs anaweza kufanya maajabu
 
Spurs anaweza kufanya maajabu
Tumuombee ila mimi simuamini kabisa.

Tuone leo tutachezaje na manyumbu.
Old trafford pamekuwa mwiba kweyu sana hata pale manyumbu wanapokuwa na wakati mgumu. Si ajabu kuona tumeshinda mara moja tu kati ya 16 pale. Kiushabiki nasema kabisa wale tutawapiga tena sana tu ila sijui huwa nini kinatokea kwetu pale uwanjani kwao.
 
Lakini Hawa nyumbuz wanatutakia Nini sisi? Kwa kikosi hiki!
Tuje kupiga mtu wiki tuonekane hatuzingatii haki ya wanyama pori?
Screenshot_20240512-173504.jpg
 
Kwa kweli hawa wakichomoka, itakuwa ni kwa misaada ya kiroho nje ya uwanja zaidi ya uwezo wa uwanjani.
Nakupa tasmini ya dakika 90+

Hadi dakika ya 40 watakua washapigwa packet 1 (kambani tatu). Nyumbu watajifanya kuja juu hapo watapigwa mbili za chap na kufanya ubao usome 5

Watagundua kwamba hapa tutadhalilika Sasa, so wataanza kujiangusha angusha, kulalamika ovyo. in short Ni upotevu wa muda tu

Japo dakika zitakua zimepotezwa nyingi, lakini zitaongezwa dakika chini ya sita ili kuwanusuru hizi nyumbu
 
Nakupa tasmini ya dakika 90+

Hadi dakika ya 40 watakua washapigwa packet 1 (kambani tatu). Nyumbu watajifanya kuja juu hapo watapigwa mbili za chap na kufanya ubao usome 5

Watagundua kwamba hapa tutadhalilika Sasa, so wataanza kujiangusha angusha, kulalamika ovyo. in short Ni upotevu wa muda tu

Japo dakika zitakua zimepotezwa nyingi, lakini zitaongezwa dakika chini ya sita ili kuwanusuru hizi nyumbu
Wako kwao hawa wahuni. Kuna namna mambo yako hovyo kwetu pale kwao. Ndo maana nikasema watapita kwa nguvu za kiroho tu.
 
Back
Top Bottom