Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kimsingi Pep ametuhofia au anataka atuue mapema. Ameingiza watu hawana fitness matokeo yake Ake ameenda kitandani
De bruyne hayupo form

Hii game Arteta ndio anailealea tu
 
Waingie

Zin
Partey
Martinel

Alie karibu na Arteta, amuambie mpira wa kunyanyasika tulishausahau sisi
Tunawaruhusu sana wazurure kwetu na hatuwakimbuzi. Kule kwa Lewis kunahitaji mipira iende tumpe wakati mdumu yule dogo
 
Mpaka dakika ya 33 City ana touches 2 kwenye boksi la Arsenal. Arsenal ana touches 6 kwenye boksi la City.

City hachezi kwa mtindo tunaoujua. Kwamba mipira wanagewa De Bruyne na Rodri kisha wanaamua mashambulizi, wangecheza hivi ingekua rahisi kwetu kutabiri mpira utaenda wapi.

Kutokana na hili Haaland amekosa huduma. At the same time Arsenal tunasakamwa na mchezaji wetu mwenye chaos kutojikuta 1 v 1 na beki. Tumejitahidi kuzuia long shots zisipigwe ila sisi pia hatupigi.

Kama tumeamua kutoshindana kumiliki mpira sioni kwanini hizo shots hazipigwi.

Mechi ya mwisho goli letu alitusaidia Ake naona leo hajataka lawama katoka mapema.
 
Tunawaruhusu sana wazurure kwetu na hatuwakimbuzi. Kule kwa Lewis kunahitaji mipira iende tumpe wakati mdumu yule dogo
Kule Ni nafasi ya martinel, na ndio mchezaji mwenye Kasi Sana tulie nae

Arteta hii game ipo mikononi mwake kabisa
 
Kuna muda mbinu zikizid mechi haivutii Bora Nyumbu wanavyochezacheza hua kuna raha yake
Ndio maana timu lenu halijielewi ...

Mpira Ni Akili ndugu ...

Ukiwa mkurupukaji kama man U ...ndio maana mnakuwa pale mlipo


Kwa sababu mnacheza Bila kutumia Akili ,kama ndondo cup ...mngekuwa mnaakili msingeshindwa kulind Goli mlilofunga ndani ya dakika 90+6min
 
Kule Ni nafasi ya martinel, na ndio mchezaji mwenye Kasi Sana tulie nae

Arteta hii game ipo mikononi mwake kabisa
Kabisa mkuu. Tungekuwa na Martinelli na wangekuwa wanamuona ( tunaupendelea sana upande wa Saka) na kupeleka mipira kule tungemnyanyasa yule dogo. Jorginho pia hapati nafasi kufanya mambo yake. Wametubana vizuri kwa kweli.
 
Rice bado ni mchezaji ambaye bei yake haitozungumziwa. Tunakosa Fluid movement ya transition kwakua Kai anakua chini au mbali na mwenye mpira ili kutransition kwa pamoja.

Jorginho yupo kwaajili ya vision na pasi ila hakuna runs za msingi kutoka kwa forwards zetu. City wana huyu kipa namba 2 na hatujaamua kumjaribu why?
 
Back
Top Bottom