


Ndugu yangu
mkorea mimi sio mganga wala mchawi ila shida ya timu yenu wala haitaji rocket science kuelewa.
Kama kweli mna nia ya kubeba makombe tafuteni kwanza kocha wa kueleweka, achaneni na hizo false hopes anazowalisha Masingeli kuhusu Mateka na takwimu zake za uchwara.
Mateka kipindi chake anacheza mpira alisha prove kua ni failure, halafu nyinyi mnategemea mpate matokeo mazuri kwa kufundishwa na mwalimu ambae naye pia alifeli, Mateka kwenye historia yake ya kucheza soka la kulipwa hajawahi kushinda kombe lolote la maana zaidi ya kombe la FA.
kiufupi Arsenyo haina tofauti yoyote na hizi shule zetu za St. Kayumba ambazo zinafundishwa walimu waliofeli secondary, matokeo yake mtoto anamaliza darasa la 7 halafu hajui kusoma wala kuandika.
Mateka ni Mid table coach, hata mentality zake unaziona kabisa ni za kufundisha Mid Table Team, humu mnadanganyana mwanzo wa msimu halafu mnapofika mwisho wa msimu mnaanza kugundua kua mna Avarage coach ambae hawezi kuwafikisha popote, matusi yanakua mengi humu halafu msimu mpya ukianza mnasahau kabisa kiini cha matatizo ya timu yenu mnakuja tena na ngonjera hizohizo, ndio maana kuna wachambuzi wakubwa wa soka hua wanawachambua mpaka mashabiki wa Arsenyani na kuwaweka kwenye level ya misukule


View attachment 2943825View attachment 2943826View attachment 2943827View attachment 2943828View attachment 2943829View attachment 2943830View attachment 2943831View attachment 2943832