Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Enzi hizo miaka ya 2000+ nikumuona Edu Gaspar anacheza wala hakua mchezaji mkali sana wazungu huita huziita "balling brains. Hizi hakuwa nazo sana kama waliomzunguka.

Ila huyu baada ya kurudishwa kwenye timu wengi hawajui ndio yuko nyuma ya usukaji kubwa wa kikosi hiki.

Ana brain na jicho kali la kufanya scouting !

Asisahaulike ni nguzo kubwa kwenye mafanikio ya Mikel.
 
PESA HIYOOOOO .!

Unalipa Pauni Milioni 105 kwa mchezaji kama huyu , sio wengine mnalipa 100 hovyo hovyo tu .!

Size ya pitch ya uwanja wa Luton ni changamoto aisee hasa kwa passing game

Kwa kiasi kikubwa hasa kipindi cha kwanza Gaby Jesus alikuwa anasaidia sana kwa Arsenal kusogea juu kwa

1: Kushuka chini , kupokea mpira na kusogea nao juu ( carries )

2: Kushambulia space baina ya outside CBs wa Luton na wingbacks wao

Luton wanastahili pongezi kwa mpango wao : walitumia faida ya udogo wa pitch kwa kubana zaidi space na kutumia counter attacks plus mipira iliyokufa kupata chochote kitu .

Kipindi cha pili ni kama vile ilikuwa nani atafunga magoli mengi zaidi ya mwenzake , mmoja anatumia ufundi wa kuweka mali chini ( Arsenal ) mwingine anatumia ufundi wa mipira mirefu na iliyokufa ( Luton ) : mwisho Arsenal wakawapa Luton ladha ya dawa yao wenyewe . Heartbreaking

NOTE

1: Yule Fullback wa kushoto wa Luton : Doughty ana mwaga maji huyo

2: Ross Barkley kama alikamia vile , kaubonda

3: Kai Havertz anakuja bhana , kajipata tayari

4: Bukayo Saka ni hatari , anafanya vitu kwa level ya juu sana

5: Gaby Jesus kuna muda anakuwa Yes kuna muda No

6: David Raya
nafikiri Ramsdale atakuwa na matumaini nafasi yake bado ipo

7: DECLAN RICE , DECLAN UBWABWA ... PESA .! What a player . Tangu atue Arsenal sikumbuki mechi gani alicheza vibaya . Arsenal waongeze zingine £20M kwa West Ham

8; Kafungwa Luton lakini wanachukia wengine .


FT: Luton 3-4 Arsenal

AMBANGILE
 
game ilikua balaa nashangaa wanaokuja uku wanasema tunashangalia ushindi kwa luton... lutona anapiga blocks kila attempt tuliokuwa tunafanya ila mtu anasma ni timu ndogo
Wamekiwasha sana, wanaanzia kukabia kwetu alafu hawachoki, hao wanaosema hivyo hawajaangalia gemu, wamecheki livescore.
 
Ben white apewe pongezi zake, kwenye maamuzi yupo haraka sana.
 
Liva kasuluhu na Luton.

Game inayofuata Luton alicheza na nyumbu.

Nyumbu akashinda 1

Luton kampiga Palace.

Ila kapigwa na Brentford.

Next match ya Luton ni dhidi ya City.

Luton akicheza na timu zinazokupa mpira na kufocus kufunga anapata tabu. Palace hakuliona hili akadondosha points zote, liva akasubiri hadi dakika ya 95 ili kupata point moja.

Timu imefanya poa. Imestep up ilipotakiwa kufanya hivyo.
 
Kuanzia 2021 mpaka leo Grealish kafunga magoli 9 tu.

Alinunuliwa 100M.

Kwanini watu hawamuoni? Kwakua City inashinda mataji.

Antony anaonekana kwakua nyumbu wapo hoi, Fofana haonekani kwakua kenge haitamanishi tena
 
Next stop A Villa at Villa Park, hapa ndio wataita maji mma kubabeeeki
Wale wanaopenda kufunguka na kushambulia...tupo hapa🤠🤠🤠....hawana beki wa kuzuia tusifunge....wataamua wao kupaki basi au tupishane....wakitaka tupishane Sasa....hapo ndo patakuwa pazuri....timu za kutusumbua sisi nilishasema ni 3 tu.... Brighton...City na Liverkuku...Hawa wengine ni watoto wadogo...sisi sio Manunu🤠🤠🤠...mpk wachezaji wanamfundisha mwalimu namna ya kukaa na wachezaji kwa amani....Leo hatulali mpk tujue hatma yenu nyny pipa na mfuniko mkicheza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…