Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kipa wa arsenal tunaemtambua ni Raya ambae ata kiungo anacheza kwa kiwango kilekile
Sisi tunamjua mwamba mdaka mishale
Ramsdale the Saviour
 

Attachments

  • IMG_20230317_133330.jpg
    IMG_20230317_133330.jpg
    59.8 KB · Views: 10
Haina noma, ngoja tuendeleze hii dozi, heshima yetu tutachukua kinguvu
Kumbuka bado hatupo Ile form ya msimu uliopita
Form ya kupokonywa ubingwa na kuambulia patupu.

Wasindikizaji FC...
Oneni timu ya Dunia liver inavyobeba makombe yote.
 
Leandro Trossard kwenye nafasi gani anajisikia vizuri zaidi akicheza:

“Hilo ni swali gumu. Sijali sana kucheza nafasi zote za juu, naona sawa. Ikiwa ni winga wa kushoto, kama tisa wa uongo, hata kama kiungo mshambuliaji, sina jibu la moja kwa moja kwa hilo.


“Nikiwa mtoto nilicheza kama nambari kumi, kama kiungo mshambuliaji au kama mshambuliaji pia.

“Siku zote huwa najitahidi kuwa kwenye eneo la hatari na katika nafasi nzuri za kufunga mabao na kwa ubora tulionao Arssnal, najua lazima niwepo, hasa nikicheza winga ya kushoto, nahitaji kuwa pale, kwa mfano. , Bukayo Saka yuko na mpira upande wa kulia, kwa hivyo nafuata silika yangu huko, kujiweka katika nafasi sahihi za kufunga mabao."View attachment 2814548
Leandro ananikumbisha enzi zangu, kasoro tu ye anatumia vyema miguu yote, mie mguu wa kulia ndio nilikiwa nautumia, mguu wa kushoto ni wa kuoandia kitandank, namba nyingi nilikuwa nacheza kwa ufasaha mkubwa mnoo, namba yangu pendwa ilikuwa ni winga wa kushoto na namba 10, ila winger ya kulia nacheza, namba 9 nabonda japo sienjoy kusema ukweli. Namba 8 ndio mama yangu nikicheza namba 8, unashangaa, kuna game tulienda kubonda sehemu namba 6 yetu tegemezi ikaumia, nikamuomba mwalimu nicheze hapo, kulikuwa na winger wa akiba(sio tegemezi) akala wiger yangu, niliupiga mwingi siku hiyo, anayofanya partey ndio yalikuwa mambo yangu, mwalimu akabaki kinywa wazi. Pengo la namba 6 halikuwepo nikaupiga mwingi game inaisha mwalimu wa wapinzani ananiomba niwe naenda kupiga nao mazoezi.

Ndio maana mie mchezaji asiye mnyumbulifu, mchezaji mgumu mgumu tu, yupo kama tren alipoelekea ndio huko huko.. Simpendi hata kidoogo kwa kweli.
 
Back
Top Bottom