Watu wanakasirika na kuchukizwa kumhusisha Mbappe na Arsenal sababu inakua ni kama kumvunjia heshima Mbappe.
Huko Ufaransa baada tu ya kuzagaa hizi tetesi wananchi wamekasirika kwelikweli, wameanzisha maandamano na kuchoma moto magari Barbarani kwa ghadhabu walizonazo, Waandishi wa habari wameamua kupindisha ukweli ionekane hayo maandamano yametokana na mauaji ya kijana mweusi ili isije kusababisha mzozo wa kidiplomasia kati ya Ufaransa na Uingereza.
Mbappe mwenyewe kusikia hizi tetesi za kuhusishwa na Arsenyau amemind kinoma.
Anasema huu ni udhalilishaji aliofanyiwa kwa makusudi, tayari amemwambia wakili wake a file kesi mahakamani ya udhalilishaji.
Muda huu tunaongea wakili wa Mbappe yupo kwa DPP anawasilisha malalamiko ya mteja wake ili ikiwezekana hii kesi ipelekwe moja kwa moja kwenye mahakama ya ICC maana mlichomfanyia hakina tofauti yoyote na uhalifu wa kivita.