FOOTBALL YA ARSENAL NI MIXA BASKETBALL

Najua unajiuliza sana hii Nini?
Kwanini wachezaji wa Arsenal Wamekuwa na aina hii ya ushangiliaji kama wanatumbukiza mpira kwenye kikapu?
Mpira wa miguu ni kuhusu UBUNIFU.Makocha mnasoma wote mnapata License A au Pro License.Lakini kinachoweza kuwatofautisha ni UBUNIFU.
Na hapa MIKEL ARTETA ameuleta mchezo wa Mpira wa kikapu kwenye kiwanja chake Cha mazoezi
Ukienda pale London Colney "Uwanja wa Mazoezi wa Arsenal" ukisema kuhusu "Basketball rule" Kila mchezaji anaelewa unaongelea nini.
Nahodha Martin Odegaard aliulizwa kuhusu ushangiliaji huu wa Basketball
anasema "Ni kitu huwa tunamzungumza sana kwenye Mazungumzo ya team.Tuna Kanuni tunazifanya ni kama zile tu Basketball
Basketball rule ni nini? Kwenye Basketball ni kuhusu kashambulia sana ndo msingi.Kutengeneza mazingira ya goli kufunga ni Muunganiko wa ufundi binafsi na team.
Kwanini Mchezo wa Mpira wa Kikapu? Na sio tennis na michezo mingine? Anasema ni kwasababu Basketball Kuna vitu Vingi inafanana na Football
Kwa mfano ambacho Basketball na Football wanashea ni "Transitions na turn overs.Na ili transition ifanikiwe Kuna vitu 4 lazima vifanyike kwa usahihi
Kwanza ni kuwa na nidhamu ya eneo.Lazima uwe kwe eneo Sahihi ili tujue wapi tunakuwekea mpira.Pili , Compactness yani kuwa kwenye umbali Sahihi ili iwe rahisi kusafirisha mpira.Tatu, Organization,yani lazima kuwe na Muundo kuwezesha shambulizi.Nne,maandalizi ya nini Cha kufanya kama shambulizi likifeli.
Na kwenye basketball mara nyingi transition ikitokea lazima mpira umalizkie kwenye kikapu.Hii utaona Arsenal wakishapora mpira wanaondoka Kwa Kasi na lazima shambulizi limazike kwa Shuti Golini.
Kitu kingine ambacho Basketball na Football wanashea ni michezo ya Uvamizi (Invasion) .Yani inahusisha team moja kuvamia goli la timu pinzani na kufunga Goli au vikapu , Lakini pia kumzuia pinzani asifunge magoli au vikapu zaidi yako katika muda fulani wa mchezo.
Mikel Arteta amediriki Kujiunga kwenye group la Whatsapp la makocha wa Mpira wa kikapu nchini Marekani NBA ili Kupata uelewa zaidi wa namna makocha wanaziandaa team zao
THIS IS FOOTBALL MADE IN ARSENAL
wilson oruma