Uchambuzi Ambangile
[emoji1593]Shape ya 3-2-2-3 wakiwa na mpira , Arsenal wameipress vizuri sana , man to man pressing . Trossard kwa Stones, Nketiah kwa Akanji , Saka kwa Ake , Vieira na Xhaka Vs Rodri na Lewis , Tierney anatoka pembeni anamfuata KDB ndani, Gabriel anatoka ndani kumfuata Mahrez pembeni.
[emoji1593]Tomiyasu Vs Grealish na Holding / Saliba Vs Haaland . Hii pressing ilifanikiwa kwasababu :-
1: Wingers wa City Grealish na Mahrez wanataka mpira mguuni badala ya ku run in behind Arsenal backline maana yake hata zile flicks za Haaland kwenye space iliyowazi hazina mtu
2: Ball carrier katikati , kumkosa Silva katikati ,pembeni ya Rodri
[emoji1593]Pep kubadilisha kuwa 4-4-2 kuingia kwa Alvarez kulisaidia kukabiliana na build up ya Arsenal , pressing ilikuwa nzuri zaidi tofauti na kipindi cha kwanza lakini pia iliongeza idadi ya washambuliaji mbele
[emoji1593]Arteta kaisuka Arsenal ambayo ipo sawasawa physically na technically , wachezaji wapo imara sana kimwili na wakiwa na mali wapo salama sana , ngumu kuwazuia kutoka nyuma na kufika mbele