hamis77
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 18,346
- 26,822
MOURINHO ALIITABIRIA MAKUBWA ARSENAL
Unaukumbuka ushindi wa Spurs wa mabao 2-0 mwaka 2020 dhidi ya Arsenal chini ya Jose Mourinho?
Nikukumbushe tu, The Gunners walikuwa wamerejea katika nafasi ya 15 na Presha ikaanza kuwa kubwa kwa Mikel Arteta kutoka kwa mashabiki lakini Jose Mourinho alikuwa na mtazamo wake tofauti.
Baada ya mchezo ule, Mourinho alisema:
“Kiufundi, Arsenal ni wazuri sana, walikuwa wamejipanga vizuri, walikuwa wanashambulia na Wachezaji wanne, wakilinda na watano.
"Halafu katika kipindi cha pili, walijaribu kutafuta pembetatu upande na walitupa shida, shida ambazo tuliweza kutatua kwa sababu wachezaji wangu walikuwa bora kimbinu"
"Licha ya hilo lakini walitupa shida kwa sababu ni timu nzuri na yeye (Arteta) ni kocha mzuri. Lakini nadhani tulistahili kushinda”
"Naweza kufikiria kesho ya Arsenal, najua kwamba vichwa vya habari vitakuwa juu yao kutokana na kutokuwa kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo, Lakini ninaamini kwa wachezaji hawa, wakiwa na Mikel, Arsenal watakuwa bora, itarudi Arsenal ya kipindi cha nyuma na watakuwa bora sana.”
Unaukumbuka ushindi wa Spurs wa mabao 2-0 mwaka 2020 dhidi ya Arsenal chini ya Jose Mourinho?
Nikukumbushe tu, The Gunners walikuwa wamerejea katika nafasi ya 15 na Presha ikaanza kuwa kubwa kwa Mikel Arteta kutoka kwa mashabiki lakini Jose Mourinho alikuwa na mtazamo wake tofauti.
Baada ya mchezo ule, Mourinho alisema:
“Kiufundi, Arsenal ni wazuri sana, walikuwa wamejipanga vizuri, walikuwa wanashambulia na Wachezaji wanne, wakilinda na watano.
"Halafu katika kipindi cha pili, walijaribu kutafuta pembetatu upande na walitupa shida, shida ambazo tuliweza kutatua kwa sababu wachezaji wangu walikuwa bora kimbinu"
"Licha ya hilo lakini walitupa shida kwa sababu ni timu nzuri na yeye (Arteta) ni kocha mzuri. Lakini nadhani tulistahili kushinda”
"Naweza kufikiria kesho ya Arsenal, najua kwamba vichwa vya habari vitakuwa juu yao kutokana na kutokuwa kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo, Lakini ninaamini kwa wachezaji hawa, wakiwa na Mikel, Arsenal watakuwa bora, itarudi Arsenal ya kipindi cha nyuma na watakuwa bora sana.”

|| Arsenal are ready to bid €20m (£17.6m) for Valladolid RB, Ivan Fresneda and beat Newcastle to his signature [Via - @Pucela_Fichajes].