Spurs wabatakiwa wafanyiwe usafi kama Chelsea inavyofanyiwa usafi sasa hivi, la sivyo hata umuweke Kocha yupi bado tu utaendelea kuona Makocha hawafai.
Kumbuka Pep Kipara alipokuja awali aliikuta Man City ikiwa Bingwa mtetezi wa EPL na pia imetoka katika hatua ya nusu fainali ya UEFA, ilisajili Wachezaji 9 msimu wa kwanza japo wanne wote walichemka (Kipa + Nolito + ....) na kumaliza ligi ikiwa nafasi ya 3 kimsimamo.
Msimu wa pili Mwa-City ilisajili tena Wachezaji 11 ndipo ikatwaa ubingwa wa EPL.
Mpira wa sasa hivi ni pesa, huna pesa utaendelea kuweweseka tu na ndicho kinachompata sasa hivi Liverpool, timu kubwa, Kocha mzuri lakini Matajiri wabahili kuliko Waha na Wapare (utani)...
