ARSENAL inaposhambulia inatumia 2-3-5 au muda Mwingine 3-2-5
Dhidi ya Sevilla ,nyuma wanabaki WHITE GABRIEL MAGALHAES NA SALIBA
ZINNY ANAPANDA NA KUWA KIUNGO AKIUNGANA NA PARTEY NA XHAKA
SAKA hutanua uwanja na kuruhusu Odegaard kuwa namba 10, pamoja na Martinell kuwa no.10 ya pili,pale ZINNY anapopanda na kuwa Winga ,Gabriel Jesus anakuwepo Kati ,lakin wanabadilishana Sana nafasi na Gabriel Martinell
ZINNY ametuongezea kitu kipya , kwakuwa anauwezo wa kucheza Kama Midfielder basi anaongeza uimara Katikati , hapa Tierney sio mzuri eneo la kiungo ,
Hivo basi mwalimu amepata option zaidi anapotaka kumtumia Zinny au Tierney.
Uwepo Wa SALIBA ,GAB NA WHITE unafanya tuwe wazuri kwenye buildup Sababu wote Ni wazuri mguuni , ukiongezea na Zinny na Partey ,hapa NDIPO unapoona nafasi finyu kwa mtu Kama Hector bellerin na Toreira
Tomiyasu huyu pia Ni mzuri Sana kwenye buildup ,hivo kwasasa mwalimu ana option nzuri upande wa kulia na kushoto , na beki za Kati ambapo White anaweza kurudi Kati Kati .
Eneo ambalo bado tunahitaji mtu Ni RW , lakin kwa uchezaji wetu niliouona , Ile namba 8 ya Xhaka tukipata mtu Mwingine pia mwenye jicho la pass na kunyumbulika basi timu yetu itakuwa imeenda NEXT LEVEL ,
Gabriel Jesus huyu anajua kutumia nafasi lakin uwezo wake mkubwa wa kucheza pembeni kulia na kushoto unawapa tabu Sana mabeki pinzani, Sababu wanashindwa kumtarget .
Goli la 2 Dhidi ya Sevilla katokea pemben upande wa kushoto , akatoa pass akawahi ndan ya box akafunga.
Pep Guardiola juzi amemuelezea G.jesus Kama Ni moja ya striker anayepress na kudefend(kuzuia) aliyewahi kumpata
Arsenal Sasa uwezo wa kupress umekuwa mkubwa Sana Sababu ya G.jesus pale mbele.