Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

STAR BOY SAKA !!

✍Baada ya kutumia energy kubwa sana Jumatano dhidi ya Liverpool , leo Arsenal hawakuhitaji kutumia sana nguvu kuwafunga Aston Villa na kukusanya alama 3 nzuri sana kwenye mbio za Top 4 .

✍Mikel Arteta aliendelea na mfumo wake ule ule 4-3-3 wenye false number 9 na namba 8 wawili ( Odegaard na Xhaka ) . Passing kwa Arsenal ilikuwa ya ufanisi sana , movements zao hasa kipindi cha kwanza ambapo kirahisi sana wangeweza kufunga goli zaidi ya moja .

✍Stevie G alichelewa sana kubadilisha muundo wake wa timu ...Coutinho na Buendia walikuwa nyuma ya Watkins huku Ramsey Luiz na McGinn katikati katika mstari mmoja ( horizontal ) ... shida ilikuwa wapi

1: Coutinho na Buendia wapo ndani sana maana yake Cedric na Tierney hawazuiwi wakiwa na mpira .

2: Tierney na Cedric wakisogea juu, inalazimika Ramsey na McGinn ndio wawafuate wakifanya hivyo wanaacha space ndani kwa Odegaard na Xhaka kuwa huru kupokea mpira na kupiga pasi mbele .

3: Mabeki wao wa pembeni ilikuwa ngumu kusogea juu ( Young na Cash ) hasa kipindi cha kwanza kwasababu mbele yao hakuna msaada na wakati huo huo Saka na ESR wame switch ON kushambulia space itakayoachwa wazi na hao mafullback wawili wa Villa .

✍ Kipindi cha pili ulihisi Stevie G anaweza kufanya mabadiliko mapema , kubadilisha kutoka 4-3-2-1 na kwend! 4-4-2 ( Buendia na Coutinho OUT ) na Traore na Bailey IN pamoja na Jacob Ramsey kumpisha Danny Ings maana yake

1: Ings na Watkins washambuliaji wawili mbele
2: Bailey na Traore wingers
3: McGinn na Douglas Luiz kwenye kiungo

✍Arteta anastahili pongezi kubwa kwa kusoma nyakati za mchezo ( Game Management ) alipoona ngumu kufunga goli la pili akaona asifungwe yeye ...kuingia kwa Rob Holding na kutoka 4-3-3 na kwenda 5-2-3 wakiwa na mpira na 5-3-2 bila mpira .

NOTE

1: Aston Villa wamepata shot on target dakika ya 94 😀

2: Kakosekana Martinelli lakini Smith Rowe kauwasha vizuri tu 🔥

3: Stevie G leo alimuonea aibu tu mwanae Coutinho ...mbrazil leo alikuwa Unga sana aisee 😀

4: ARSENAL WANADAIWA ALAMA 5 TU DHIDI YA CHELESEA NA WAMEWAACHA UNITED KWA ALAMA 4 NA MCHEZO MMOJA MKONONI...

✍Arsenal wanaweza kuwafikiria Chelsea zaidi kuliko Man United West Ham na Spurs.

AMBANGILE
 
If I was Arteta, I'd tell England Saka is injured, after getting no protection in this game, and to shove their friendlies up their hole.
 
Tatu Muhimu

Mojawapo Ya Game ngumu Tulizocheza na hii pia ni Mojawapo Haswa Ukizingatia Uchovu wa Kucheza J2 na J5 Usiku na Leo ni Jmos sa 6 ya Kule Uingereza...Tumeona Jinsi Vijana Wanavyopambania Team kwa Umoja na kwa Ushirikiano na Nidham ya Hali ya juu
Napenda jinsi Tunavyozuia haswa mipira ya juu Kuanzia Cross Corner na Set pieces...Hatuzuii kwa ubora wa Asilimia Mia ila Ni ngumu Sana kutushambulia mpaka ukutane na kipa haswa hizi mid table team ...

Sasa hivi ukiiangalia Arsenal Inacheza unaona kabisa kocha kaitengeneza team kila idara inaonekana uwanjan na hata kwenye kucheza unaona ushirikiano kuanzia Defensi midfielder na Foward Kilichobakia ni Kuongeza tuu Quality na quantity..
Game ngumu Mwanaume GABRIEL MAGHALHAES kasimama Vyema Pale nyuma Kudominate kila kitu kuanzia Cross Corner Clearance na blocks ...Sisemi Wengine hawajacheza Vyema ila Mwamba kasimama imara kwel kwel kwenye hatari nyingi zilizoelekea langoni mwetu..
Vijana wetu wanastahili pongezi kubwa mno maana walikuwa na uchovu na pia wamejitahidi kuondoa ile dhana ya kuanza kupoteza game baada ya game skuiz skuiz hata tukifungwa tunarudi haraka kupata matokeo mazuri tofauti na miaka kadhaa nyuma tulikuwa wakati wa muhimu kama huu tunakata moto mapema.

Next Game Palace vs Arsenal @ Selhust Park.
1647639962924.png
 
Aaron Ramsdale miss Arsenal’s match against Villa today, after sustaining a hip injury during the 1st half vs Liverpool.


Player hoped to play but medical advice prohibited.


Likely to miss #ENG camp to recover. . #AFC
@TheAthleticUK
 
Tunarudi UCL sio? Kama tajiri anapromise kuwapa wachezaji zawadi wakifuzu UCL vipi kuhusu usajili? Natumai tutakuwa na a big summer window. Oya hapo tutakuwa balaa zaidi.
stan alishaahidi toka kipind cha emery ,timu ikirud UCL anamwaga hela, alimpa emery paun mil 200, akazingua, now arteta kashatumia paun mil 200, ukweli ni kwamba wengi wanamchukulia stan kama ana miaka mingi arsenal, ukweli ni kwamba toka aichukue timu 2018/2019 kwa 100% mwanae josh amekuwa karibu na timu

juzi wenger amesema toka tuhamie emirates, kipind hiki klabu imetoa hela,
 
I rarely go to vibanda umiza, Leo nilikuwa huko, ndio maana hata typing yangu ilikuwa hovyo kwa sababu nilipiga Martin bianco za kutosha. Thanks God we have passed what many thought was a difficult hurdle. I believe this win has disturbed many currently dreaming of top four. But Arsenal is not aspiring to be in top four, tunatafuta nafasi ya chelsea
 
Aston Villa manager Steven Gerrard speaking to BT Sport: "It was a tough first half because we allowed it to be tough. I think we were indecisive in the things we tried to do. I think our performance lacked belief. It wasn’t until after half-time that we showed we can be better.

"We deserved to be behind in the first half. We were second best. We set up to be aggressive but lacked belief in what we were doing. I thought certain individuals lacked belief. It’s hard to execute a game plan if not everyone believes in what you are doing.

"We were less indecisive in the second half and off the back of that created four interesting moments. The performance was a lot more positive.

"The league doesn’t lie. Certain teams are ahead of us at the moment and there’s a reason for that. We’ve got to grab it off them, believe in what we’re doing and get support from up above.

"I’m emotional, I care, I don’t like getting beat."
 
Steven Gerrard on Mikel Arteta:


"You’ve got to give people at Arsenal credit for supporting him, backing him and giving him the time to stamp his identity.. defensively, they’ve improved. Set-piece wise, they’ve improved. Credit to the coach and his coaching staff."
 
Hakuna Process mzee, zaidi tufurahie tu Ushindi. Kuufunfibsitarajii Teta aje kuwafunga Pep na Jurgen, na kushundwa kuwafunga hao ni mark time ya kuukosa Ubingwa jama kawaida.

Ka muhimu kwa sasa no return of we are the champion night basi
Arsenal tulivyochukua community shield msimu wa nyuma kocha wa Arsenal alikua nani na wa liva alikua nani?
 
Back
Top Bottom