Haya ndiyo matokeo ya kuchezea shilingi chooni. Kwa matokeo haya tayari tuko nje ya mashindano haya, hivyo inabidi kupata goli moja au zaidi ili kuweza kuendelea.
Hiyo defensive game ndiyo imetuadhiri, sasa hivi lazima tu tushambulie kwa nguvu zote na pia kuhakikisha jamaa hawaoni tena nyavu zetu, maana siye draw tu inatutosha kusonga mbele.
fAB siwezi kumlaumu sana, tumezidi pasi za kusakiziana. Tumechukua mpira vizuri badala ku-clear mtu kaenda kumpa pasi fab wakati wachezaji wa barcelona kibao wako pale, matokeo yake hakuwa na jinsi zaidi ya kubahatisha kisigino. Ndio maana mwanzo nikasema bora tulibutue tu mpira mbele waanze upya kushambulia kulikoni kujaribu kutoleana pasi goli kwetu na kupoteza.