Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Usajili Arsenal hawa ikifika kesho hawatakuwepo Arsenal.

Joe Willock- Newcastle United (England) usajili kamili

Reiss Nelson- Feyenoord (Holland) mkopo na huenda akarudi msimu ujao.

Willian- Corinthians (Brazil) mkopo na baadae usajili kamili

Hector Bellerin- Beal Betis (Spain) mkopo na baadae usajili kamili.

Alex Runarsson - OH Leuven (Belgium) mkopo na baadae usajili kamili.

Na William Saliba na Matteo Guendouzi Marseille (France) mkopo na huenda akarudi Arsenal January au msimo ujao.

Lucas Torreira yupo Fiorentina Italy kwa mkopo na baadae usajili kamili.

Mohamed Elneny na Ainsley Maitland-Niles bado ni wachezaji wa Arsenal.

Ainsley Maitland-Niles ameadhibiwa kwa kufanya mazoezi peke yake baada ya kuandika ujumbe IG kutaka uhamisho.
 
Takehiro ni CB ila anachezeshwa RB.

Linarudiwa kosa la Chambers hapa.
 
Takehiro ni CB ila anachezeshwa RB.

Linarudiwa kosa la Chambers hapa.
Hapana ni "versatile" yaani hucheza nafasi zote.

Tottenham hawakumchukua kwa sababu ya lugha na wameenda kumchukua Emerson kwani yeye na kocha Nuno wataelewana lugha ya kireno.

Angalia video ya mechi ya olimpiki ambapo Japan waliifunga France 4-0 na Tomiyasu alicheza kama beki wa kulia.

Mabeki wa Japan wengi ni "versatile" na hata beki wao wa kushoto Sakai kwenye mechi na Mexico alicheza kama beki wa kulia na hii mechi na France akacheza kama beki wa kushoto.
 
Chambers siyo versatile?

Beki CB na full backs hawawezi kufanana na hii ni kwakua wana sifa tofauti. LB kucheza RB au vice versa ni sawa kwakua hizo nafasi za fullbacks zinahitaji sifa sawa.

RM na LM ni sahihi zaidi kuwatumia kama full backs kuliko hata CB
 
Calum Chambers aliumia goti mechi tulopoteza na Chelsea december 2019.

Tangu pale ana tatizo la consistency kwenye kukimbia na khasa upande wa kulia.

Ndo maana wameamua kuchukua beki mwingine wa kulia.

Bellerin nae hivyohivyo ana majeraha ya goti yanojirudia hivyo Arsenal wamekuwa na tatizo la kumpata beki wa kucheza msimu mzima bila kuumia.

Hivyo nafikiri huyu Takehiro na Maitland Niles wanaweza kutumika upande wa kulia kama first choice defenders.

Cedric Suarez ni beki wa hovyo sana na hafai hivyo nae wavuta mkataba wake uishe mwakani.
 
Soares siyo beki wa hovyo
 
Toa fact kwa nini cedric ni beki wa hovyo mkuu
 
Soares siyo beki wa hovyo
Unamaanisha anacheza kwenye mfumo wa hovyo,yuko kwenye mbinu za hovyo,yuko chini ya kocha wa hovyo au kazungukwa na wachezaji wa hovyo?

Samahani castr you are far better than me ila matokeo ya timu yananivuruga
to the fullest.na usajili wa kina tekehiro ndo basi daah.
Ila live and love football kwa hiyo haya maumivu ambayo wapinzani wanahisi tunapata its only about fantas
 
Nakumbuka kaka
 
Mkuu,

Mtu kama ni mjinga hatuna namna isipokuwa kumuita mjinga. Call a spade a spade bro.

Mengine yote nimekuelewa. Thanks
 
Hapa ndio nakataa bro. Hahahahahaahah

Hizo £123M ni kocha wako ndio aliosema zitumiwe kwa Tavares na wala sio Kroenke hahaahahahha
 
Cedric hawezi ku-track back akipoteza mipira na hivyo kuwa uchochoro kwa timu pinzani.

Takwimu za mechi na Man City Soares alipoteza mipira mara 8, alitoa pasi 7 tu, hakuzuia mipira yoyote ile, wala kujaribu "tackles" na mipira ya juu alishindwa kuzuia mipira mitano.

Pasi zake hupotea na humlazimu kuanza kurudi nyuma alikokuacha hakuna cover.

Alipoingia Maitland Niles alifanya uzuri kwa kuzuia mipira mingi na kutoa pasi za uhakika ingawa ilikuwa too late.

Mechi na Chelsea ilikuwa ni hivyohivyo.

Hivyo nafasi ya beki wa kulia ni Takehiro na Maitland Niles ndo wawe first choice.

Bado wadogo na wepesi kukimbia kuliko Soares mwenye umri wa miaka 29 sasa.
 
yani Richard unatujaza kama Aroon arsenal
Arsenal sasa hivi wanafanya Project na wanachukua vijana ambao ukiangalia umri ni kati ya miaka 20-23 ukindoa Auba na Laca na wengine kama Soarez.

Ni project ambayo ni lazima afanikiwe na Arteta amepewa mechi 13 aokoe kazi yake.

Ndo maana wenye timu wanamwangalia tu na kutoa mpunga.

Hadi jioni hii Arsenal itakuwa imetumia jumla ya pauni milioni 150!

Ila Wameokoa mishahara ya kijinga kwa watu kama Willian na wale wachezaji ambao wapo timu zingine kwa mkopo ambapo timu husika ndizo zinalipa mishahara kwa kugawana na Arsenal.
 

Mkuu kwenye Football nowadays you cant attack if you cant defend, Attack inatengenezwa kuanzia nyuma ndio maana shauku yangu kubwa ni Leno kuwa second choice. Arsenal yetu aerial duels hatuwezi kucheza halafu unakuta GK anaGo long anytime..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…