Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

kila watu waanzie walipoishia msimu uliopita
yamepigwaaaaaaaaa
😀😀😀😀😀
 
Mkuu salama? Pole kwa kipigo cha jana.

Hili jambo mbona nimeeleza humu mara nyingi tu, kabla ya kumpa kazi Arteta Arsenal wali approach high profile coaches kama Allegri, Luis Enrique nk na wote iliwashindwa sababu ya mahitaji yao ya pesa za kufanya squad overhaul.

Arteta ni kocha asiye na experience kwa hiyo kama Arsenal waliona anafaa lazima umpe vitu viwili, 1. Time to establish himself 2. Resources.

Tazama PSG pamoja na kikosi chao bado wanasajili Messi, Ramos, Donnouramma nk in the same transfer window na wana Pochettino kama kocha.

Man City bingwa mtetezi wa ligi na bingwa wa Carabao anasajili Grealish na bado wanamuwinda Kane to bolster their squad, kwenye bench kocha ni Pep.

Chelsea ambaye ni bingwa wa Uefa na Super cup ananunua Lukaku na bado wako busy kwenye transfer market kuongeza watu kwenye kikosi chao na hapo kocha ni Tuchel.

Huyu Arteta na hawa kina 'Lokonga' kama wanavyo tunanga wapinzani wetu unataka kumlaumu kwa kipi labda?
Angalau tutajadiliana ki-mpira.


Hili jambo mbona nimeeleza humu mara nyingi tu, kabla ya kumpa kazi Arteta Arsenal wali approach high profile coaches kama Allegri, Luis Enrique nk na wote iliwashindwa sababu ya mahitaji yao ya pesa za kufanya squad overhaul.
Naomba ushahidi wa hili usio na shaka ndugu yangu, kwamba hao makocha hapo juu uliowataja walikataa kwa sababu ya mahitaji yao ya pesa. Kama huna hii itakuwa ni story tu za vijiweni.

Lukonga amesajiliwa kwa fedha, Guendouzi ameondolewa kwa mkopo (pengine tunalipa part ya salary), hili unadhani ni kosa la tajiri??

Ben White amesajiliwa kwa £50M, Saliba hakupewa hata nafasi ya game hata 1. Something is really fishy here bro, hili unadhani ni kosa la tajiri?? Why not use Saliba from the first place uende umsajili White???

Ninachokiona ni kwamba Edu na arteta wanapiga hela kimya kimya na nadhani tajiri ameshtuka juu ya hilo.

Madrid wanaenda kutupiga pesa za kutosha kwa odeegard ambae hatumuhitaji. Hahitajiki Odeegard, Arteta kwa chuki zake tu na udhaifu wake akamuondoa alie Bora Martinez na kumuacha Leno je hilo nalo ni kosa la tajiri?? Tukiangalia in the past five years miongoni mwa timu zilitowa peas nyingi kwa ajili ya usajili pale EPL utaikuta Arsenal IPO pengine ndani ya top 5. Tunamlaumuje tajiri hapo??
 
Angalau tutajadiliana ki-mpira.



Naomba ushahidi wa hili usio na shaka ndugu yangu, kwamba hao makocha hapo juu uliowataja walikataa kwa sababu ya mahitaji yao ya pesa. Kama huna hii itakuwa ni story tu za vijiweni.

Lukonga amesajiliwa kwa fedha, Guendouzi ameondolewa kwa mkopo (pengine tunalipa part ya salary), hili unadhani ni kosa la tajiri??

Ben White amesajiliwa kwa £50M, Saliba hakupewa hata nafasi ya game hata 1. Something is really fishy here bro, hili unadhani ni kosa la tajiri?? Why not use Saliba from the first place uende umsajili White???

Ninachokiona ni kwamba Edu na arteta wanapiga hela kimya kimya na nadhani tajiri ameshtuka juu ya hilo.

Madrid wanaenda kutupiga pesa za kutosha kwa odeegard ambae hatumuhitaji. Hahitajiki Odeegard, Arteta kwa chuki zake tu na udhaifu wake akamuondoa alie Bora Martinez na kumuacha Leno je hilo nalo ni kosa la tajiri?? Tukiangalia in the past five years miongoni mwa timu zilitowa peas nyingi kwa ajili ya usajili pale EPL utaikuta Arsenal IPO pengine ndani ya top 5. Tunamlaumuje tajiri hapo??
Kuna kocha tulihusishwa naye kabla ya Arteta ila sidhani kama hata alikua approached.

Hili la Saliba niliwahi lisema humu. Saliba na Fofana wametoka timu moja ambayo hiyo timu Saliba ni nahodha, kitakwimu Saliba kamuacha mbali Fofana na wa kwanza kuja EPL alikua Saliba.

Fofana amekuja ndani ya wiki mbili anagewa namba Leicester huku Arsenal wanasema Saliba hayupo tayari.

Kisha Saliba akarudi ligue 1. Mpaka ligi inaisha nafikiri hakuna aliyefanikiwa kumpita kwa kudribble.

Guendouz ana attitude nzuri. Shida yake ambayo kila siku naisema ni hana chochote kitakachomfanya awe starter day in day out, stamina hana, pace hana, skills hana, vision hana. Notice kwamba Emery kamtoa daraja la pili (au la tatu) Lokonga sijamuona akicheza ila stats zake zinaongea vizuri. Sidhani kama tumepotea kwa Lokonga.

White usajili wake ni wa kuziba pengo la Luiz ambaye kwa Arsenal alikua ndiye beki anayeweza piga long balls kuzidi waliokuwepo. Na White anaweza hizo long balls so usajili wake ni ule wa kutaka timu icheze kuanzia nyuma. (Maelezo siyo yangu)

50M is ridiculous but wote tunajua katika negotiation kuna vitu vinaangaliwa. Muda uliobaki katika mkataba, umri wa mchezaji na timu yake inamuonaje.

Odegaard kuanzia amekuja mpaka ameondoka ametengeneza nafasi nyingi kuzidi aliowakuta lakini kiukweli mi naona Odegaard ni mchezaji ambaye hakufanya nilichotarajia. Ama hivyo au kocha hajui jinsi ya kuextract potential ya mchezaji skilled kama yule.

So kwangu ni mchezaji ambaye ni bora aje tena ila kwa mkopo na option ya kununua iwepo ikatokea kuna vitu ametimiza.

Tuna Leno. Tumemaliza msimu timu ya tatu kufungwa magoli machache. Tuliowauzia Martinez wako wapi? Varane kwa pesa aliyouzwa imeonekana Madrid ni wajinga lakini wangekaza shingo angeondoka free kama Ramos na kama donnaruma. Na sisi yangetukuta. Martinez anahitaji kua starting XI ili apate namba Argentina.

Sidhani kama Arsenal haitakua nje ya top 7 lakini hata kama itakuepo unadhani gape la kutoka walio juu yake mpaka yeye litakua lipoje? City katumia almost 1B United katumia almost 1B.

Arsenal atakua katumia sh ngapi? Madirisha ya usajili mangapi arsenal alitangaza kua na 200M za usajili? City anasajili beki wa 60M anagundua ni kinabo, anasajili wa 40M anagundua ni kinabo anasajili wa 20M ndiyo anakua stopa ile 100M inaachwa ipashe joto benchi.

Ni kama darasani niwe wa pili katika matokeo ila nina 30 wakati wa kwanza ana 80, haimake sense. Kua wa pili won't matter kwa gape kama hilo.
 
Hii team inachosha yaani hiki kitambi changu nilicho kipata ndani ya miezi mitatu hii, kitapotea ndani ya wiki moja, hapo bado Chelsea na City daaaaah.......

Hivi huyu Kroenke anatutakia nini si aondoke manake anang'ang'ania timu na hataki kuweka hela,yaani kama ikiwezekana wamloge atuachie timu yetu.

Tutamlaumu Arteta sawa lkn hata akija kocha mpya still hatopewa fungu la kutosha la usajili.Yaani mashabiki wa Arsenal kwa sasa tulivyo ni kama wale wasabato masalia waliotaka kusafiri ulaya bila passport wala nauli,tusijipe imani timu hatuna, kocha hatuna na Kroenke mbahili.
Screenshot_20210814-170334_Chrome.jpg
 
Washabiki ya hii timu mna moyo wa Uvumilivu kushindaa Mtu anaenyongwaa hadharani
 
Analaumiwa kwa kuchagua kununua substandard players, na kukubali kufanya kazi ambayo haiwezi, vinginevyo angekataa offer ya kibarua
Ha haaaa, mkuu kwa Arteta ile ni offer ambayo asingeweza kuikataa hata kama 'kiatu kinamvuka', hata ingekuwa ni mimi ningejilipua kutest zali.
 
Oya nyie mtamuua mzee wa watu Paul Kagame

We just must NOT excuse or Accept mediocrity. A team has to be built with purpose to win win win. So that when we lose....it was not to be expected! I am sure we all know on whose shoulders the heaviest burden rests. I hope they know too or even accept it!!! End
 
Naomba ushahidi wa hili usio na shaka ndugu yangu, kwamba hao makocha hapo juu uliowataja walikataa kwa sababu ya mahitaji yao ya pesa. Kama huna hii itakuwa ni story tu za vijiweni.
Mkuu kwa kunidai ushahidi usio na shaka utakuwa ama umedhamiria kunizuia kujadili au umeamua 'kunikomesha' tu, ha haaaa!!

On a serious note, taarifa zilizoripotiwa na media zenye kuaminika kwa habari za michezo ikiwemo goalnews.com ziliripoti kuwa Luis Enrique alihitaji £250m za usajili huku akieleza kuwa ni wachezaji sita tu wenye uhakika wa kupata namba kikosi cha kwanza na wengine watahitaji kuraise their standards to convince him.

Lukonga amesajiliwa kwa fedha, Guendouzi ameondolewa kwa mkopo (pengine tunalipa part ya salary), hili unadhani ni kosa la tajiri??
Hii ni normal situation kwa vilabu vingi tu, kama hujaweza kumuuza mchezaji usiemtaka kikosini, kuliko kukaa naye umlipe full salary ni more economy kumtoa kwa mkopo then mnashare salary huku akipata game time kutunza/kukuza uwezo wake na thamani yake pia ili hata ukitaka kumuuza upate hela nzuri.

Ben White amesajiliwa kwa £50M, Saliba hakupewa hata nafasi ya game hata 1. Something is really fishy here bro, hili unadhani ni kosa la tajiri?? Why not use Saliba from the first place uende umsajili White???
Hili pia ni kawaida anapokuja kocha mpya, wapo wataondoka, wapo watabaki na wapo wa bench wataaminiwa kutokana na philosophy ya kocha husika, by the way Saliba hakusajiliwa na Arteta.

Ninachokiona ni kwamba Edu na arteta wanapiga hela kimya kimya na nadhani tajiri ameshtuka juu ya hilo.
Hili acha na me nikurudishie 'kibano' ulichonipa hapo juu, naamini huna ushahidi usio na shaka, ha haaaa!!
Madrid wanaenda kutupiga pesa za kutosha kwa odeegard ambae hatumuhitaji. Hahitajiki Odeegard, Arteta kwa chuki zake tu na udhaifu wake akamuondoa alie Bora Martinez na kumuacha Leno je hilo nalo ni kosa la tajiri??
Kupigwa hela inaweza kutokea hasa kwenye situation tuliyopo (panic buy), lakini nayo imetokea watu wanalipa £50m+ for bench warmers. Katika hiki kipindi cha mawakala hilo linaweza kukukumba, sometimes mawakala wanawezesha deal kwa maslahi yao na sio vilabu.

Issue ya Martinez nadhani alipata nafasi kama mechi 7 hivi za mwisho baada ya Leno kuumia, unawezaje kumuamini kirahisi hivo kwa mechi 7? Huyu Martinez alikuwepo enzi za Wenger, Unai na hakuaminiwa kupewa namba. Infact Leno alinunuliwa kuwa namba 2 nyuma ya Cèch na yeye akiwemo, sasa mnatakaje Arteta amuamini kirahisi tu?

Tukiangalia in the past five years miongoni mwa timu zilitowa peas nyingi kwa ajili ya usajili pale EPL utaikuta Arsenal IPO pengine ndani ya top 5. Tunamlaumuje tajiri hapo??
Tangu Kreonke achukue club hajawawi ku endorse pesa, hiyo unayoisema nyingi ni ambayo club imezalisha toka kwenye vyanzo vyake vingine.

Hizo pesa kweli ni nyingi lakini not well spent, unaweza kuwalaumu wanaonunua wachezaji lakini ukienda deep utagundua deals zetu nyingi hata cash hatuwezi kulipa tunalipa kwa installments, huo utaratibu wa malipo ambao timu nyingi haziutaki zimetufanya tushindwe kupata top target players ila tunanunua wale ambao wanakubaliana na taratibu zetu za manunuzi and that's down to the owner (Kroenke).
 
Back
Top Bottom