Mara ya mwisho Slavia Praha kufungwa ni tarehe 10/12/2020 Arsenal mara ya mwisho kufungwa ni jana tarehe 18/03/2021. Walifungwa na Bayer Leverkusen Europa, wiki nyuma Slavia alikua amempiga Leverkusen moja kwa bila.
Slavia amemtoa Leicester kwenye mashindano, Slavia pia ndiye kakomesha hii run ya Rangers kutofungwa kwa mechi zote tangu msimu uanze. Hatuna historia nao ndefu, mwaka 2007 tukiwa Europa hatua ya makundi tulimfunga Slavia 7 kwa bila kisha second leg tukatoka naye suluhu ya bila bila.
Slavia ya 2007 ungemwambia shabiki wake kwamba kuna msimu utafika hawatofungwa na wataitoa Europa timu iliyo ndani ya top four Epl asingekuelewa but here we are. So ingawa inatakiwa ionekane game nyepesi ila hii siyo Arsenal ile hii ni Arsenal ambayo ina presha, haina wapeleka mipira mbele na watengeneza chansi wa kutosha.
So tuna kazi ndefu kiasi chake, gemu zetu mbili za Europa zilizopita zimeonyesha jinsi gani bado Arsenal ina shida kucheza kama kikosi, swala ambalo Slavia hawana tatizo nalo. Tutakutana nao 08/04/2021 hapa kati kati tuna kesi za EPL tunahitaji kubadilika haraka kama tunataka tuongeze chansi yetu ya kuongeza step towards glory.