Kufukuza kocha siyo issue. Issue ni picha kubwa inayoambatana na kubadili kocha. Timu inapobadili kocha inabidi ijue pia itapaswa kuingia kwenye mradi mpya wa usajili. Mfano mzuri ni Liverpool. Walipoamua kuingia kwenye project mpya (2015) walitafuta kocha anayeendana na wanachotaka. Wakaanza kumpa kikosi anachotaka taratibu.
Imewachukua Liverpool misimu minne kuanza kuvuna walichopanda. Klopp hakuanza kupata mafanikio mpaka pale alipopata mchezaji wa mwisho aliyemtaka (kipa). Ungedhani kuwa Liverpool iko tayari kushindana baada ya kumsajili VVD, lakini bado kipa aliwaangusha. Walianza kutwaa mataji baada ya kuleta kipa ghali zaidi duniani wakati wakimsajili.
Angalia Spurs (japo wengi mnawadharau ila project yao ni master class). Baada ya kukamilisha project ya uwanja na kwamba project yao ya awali na Poch (ya wachezaji 7; akina Son, Dele, Kane, Lamela, Dier, nk) ilikwisha anza kuzeeka wakaamua kuingia kwenye project mpya ya kujenga kikosi.
Lakini walijiuliza ikiwa Poch ndiye kocha sahihi kulingana na malengo yao. Wakaona wamfute kazi kocha aliyetoka kuwafikisha fainali ya uefa ambayo hakuna aliyetarajia! Wakaona wamwajiri Mourinho lakini wakijua fika atataka kikosi chake.
Levy alimbipu Jose kwenye dirisha la January kwa kumpa wachezaji wasio chaguo lake. Jose hakujibu akaacha wajijibu wenyewe (kati ya sajili tatu; Bergwijn, Gedson na Lo Celso, ni moja tu inayofanya kazi, ya Lo Celso).
Dirisha lililofuata wakampa wachezaji 7 wapya na sasa Spurs ndiyo timu inayoogopwa zaidi (kimatokeo: achana na habari za beautiful football). No dhahili pia kuwa January ijayo watampa anachotaka yaani beki ya kati inayocheza kuchoto.
Ukijumlisha sajili za mwaka mmoja wa kwanza wa Jose ni wachezaji 10!
Sasa swali kwenu Arsenal mnaotaka Arteta aondoshwe, je timu yenu ina ubavu na utayari wa kumpa kocha mpya kikosi anachotaka? Kama jibu ni hapana basi mjue atakuja kocha mpya, atapewa wachezaji wawili watatu ili mgt ijivue lawama kisha naye hamalizi misimu miwili.
Huo ugonjwa wa poor planning ndiyo pia unaitafuna timu yangu ya zamani. Na yenyewe tangu babu astaafu malengo yake ya msingi ni kukuza zaidi biashara kuliko soka huku wakifanikiwa kuwahadaa mashabiki kwa kujificha kwenye kichaka cha "beautiful attacking football".