WACHA NIKUPE MADINI MAPYA AMBAYO EPL CLUB WANACHOTAKA KUKIFANYA
Rolland Walter Barbosa
Klabu kubwa Mbili ambazo ndizo msingi wa soka la Uingereza Liverpool na Manutd wameandika proposal mpya Ambayo itakuwa dira ya Soka la Uingereza kuanzia katika Uwanda wa Premier league mpaka madaraja ya Chini kabisa mwa League zilizopo nchini England huku tayari kukiwa na support ya team 6 kubwa ambao inaonekana watayabariki mabadiliko hayo yanayoitwa *PROJECT BIG PICTURE*
1.Mabadiriko ya Muundo wa League na Kushusha team Kutoka team 20 mpaka kuwa team 18 ambapo Maamuzi makubwa ya league yatakuwa chini ya Vilabu vikubwa sita(6) ambavyo ni Liverpool,Manchester United,Arsenal,Chelsea,Mancity na Tottenham Hotspurs.Huku kukiwa na mabadiriko katika kura zenye nguvu ya kimaamuzi ambapo Kwa sasa huwa zinahitajika Kura 14 katika kuamua kitu na badala yake ita shift kwenda kula 9 na Katika kura 9 hizo zitajumuisha team kubwa 6 na team 3 ambazo zimecheza muda mrefu katika Premier league ambapo kwa sasa team hizo 3 ni Southampton Newcastle na Everton.
2.Kila mwaka kutakuwa na kiasi cha £250m kitakachopelekwa kwa madaraja ya Chini kwa ajili ya kuwasaidia kutokana na athari za corona hizo zitakwenda moja kwa moja kabla ya msimu na 25% ya mapato yote ya Premier league watapatiwa mwishoni mwa msimu huku kiasi cha £100m kikienda kwa shirikisho la soka Nchini England Fa.
3.Kufutwa kwa Michuano ya Carabao Cup na Community shield japo Michuano ya Carabao inaweza Kuwa inachezwa na team ambazo hazitokuwa zinashiriki Michuano ya Ulaya.
4.Team 2 Ndizo zitapanda daraja kutoka Championship moja kwa moja na team ya 3,4,5 ktk msimamo basi zitapambana na team ya 16 katika league kumsaka mshindi wa Playoff kuchukua nafasi ya 3.
5.Team 9 katika Epl zikiwamo team 6 kubwa zitahusika moja kwa moja na maamuzi ya kiuendeshaji na mabadiriko ya league pia kucheza michezo zaidi katika michuano ya Uefa ambayo kuelekea 2024 kunaweza kuwa na mabadirko makubwa zaidi.
6.Wakati Epl Ikiwa na
team 18 league zingine za madaraja ya chini zitaendelea kuwa na team 24 kama ilivyo mwanzo.
7.Katika Mipango hii Pia hakutakuwa na gawio kubwa kwa wakubwa 6 bali ni pendekezo linaloonesha kuwa Hakutakuwa na tofaut kubwa ya kimapato kwa team za league kuu na Football leagues(Efl).
8.6% ya mapato yote watakayopata Premier league basi yatakwenda katika uboreshaji wa Viwanja vya madaraja ya chini yote kila mwaka.
9.Kutakuwa na taarifa za wazi kabisa ambazo za mapato na matumizi zitakazo simamiwa na Fa kutokea sheria za Uefa so kwa sasa unaweza pata Rungu kupitia Fa.
10.Kutakuwa na Bei kuu ya mashabiki watakao kwenda viwanja vya Ugenini ambapo inategemewa iwe £20 per ticket.
11.Msimu wa League kuanza mwezi wa nane (August) na katika kila miaka 5 basi kutakuwa na Michuano inayoitwa Summer premier league Tournement.
12.Pia mabadiriko ya Mfumo mzima wa Ukopeshaji wa Wachezaji ambapo wachezaji 15 wanaweza ajiliwa na klabu moja kwa Mkopo katika level yeyote ile ila unaturuhusiwa kuwa na wachezaji wa 4 pekee tokea klabu 1.eg Southampton apate wachezaj wa 4 toka Mancity wa mkopo.
Sent using
Jamii Forums mobile app