Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kuna stats zake niliandaa jana wakati nakujibu hii comment, kwa bahati mbaya wakati naandika tukapata ajali mbaya ya bus hiyo simu ikapotea kwenye hilo tukio.
 
Ni wapi nimeonyesha hapangwi kwa kuwa yeye ni muislam?? Mkuu tafadhali sana usiniwekee maneno kinywani mwangu. Nimesema issue za ozil ni political. Ni off the pitch issue. Hebu nionyeshe nliposema hapangwi kwa kuwa yeye ni Muslim.

Huo utakuwa ni ujuha wa hali ya juu tukitaka kuanza kupanga kikosi kwa kuangalia dini za watu.

Nimesema ozil ameona issue isiyo ya sawa akaamua kupaza sauti na atasimamia anachokiamini mpaka mwisho wake. Done!!!!

SIJASEMA HACHEZESHWI KWA KUWA YEYE NI MUSLIM
 
Tuelewane.

Siyo hapangwi kwakua muislamu au hayupo form. Ni hapangwi kutokana na ishu za kisiasa zaidi za nje ya uwanja.
Na hichi ndicho nlichokisema au wengi tunachokisema.

Jamaa aniombe radhi aiseee. Asitake kunisingizia
 
Kuna mdau hapo juu anataka pepe aanze against city kwa sababu pepe anauwezo wa kukaa na mipira (holdup play).

Hii kazi baada ya kuondoka Giroud basi mtu anaeiweza zaidi ni lacca kwa pale kwetu
 
Duuuh. Mimi huwa namuona kama akifika mbele anafanya masihara. Cross zinagonga mabeki, akipigiwa through pass hamalizii, saa zingine hamtoki beki akimpiga chenga na inakuwa kama mbio zake ni za bure. Kumbe anafanya vizuri tu. Je hii ni ubora wake au udhaifu wetu kwenye kutengeneza nafasi za kufunga kupitia viungo na washambuliaji wetu? Naona kama anacheza chini ya kiwango chake halisi. Anatakiwa kuwa anafunga sana tu na kutoa assists.
 
Ok
 
Sawa
 

Sensible piece of writting,I dont know what came over him, but it has left a lesson to the club. I hope next time they draft a contract with any incoming player, they will include clauses that will deter the bad behavior shown by ozil. Hopefully it will be difficult for him to secure any decent contract, I was his fan, but I have written him off
 
Nadhani hata hali ilivyo sasa bado club ingeweza kumfungulia law suit Ozil, ameleta madhara makubwa sana kimapato na mahusiano ya club na jamii mbalimbali. Nahisi ni busara tu imetumika kumuacha, maana akidaiwa kufidia damage alizoleta atafilisika kila kitu.

Jamaa amenisikitisha sn vitendo vyake, hana professionalism kabisa. Sijui hata km ana watu wa kumshauri, eti juzi anajitolea kumlipa yule katuni wa Gunners ambaye analipwa $1000 huku kasababisha loss za mabilioni kwa club, Ozil ni aina ya watu flani masnitch sn afu anajipaka rangi mbele za watu.

Kama ulivyosema sidhani kama atapata deal ya maana baada ya kuondoka Arsenal kwa sababu ni club gani iliyo tayari kuingia mgogoro na soko la China kwa zama hizi?
 
Siku zote watu wakweli, wanaosimamia haki, wasioupenda utumwa, wenye msimamo na wanaosimamia wanachokiamini pia wasiopindishwa na kupelekeshwa na watu! Huonekana jeuri, kiburi na wakorofi.
 
Siku zote watu wakweli, wanaosimamia haki, wasioupenda utumwa, wenye msimamo na wanaosimamia wanachokiamini pia wasiopindishwa na kupelekeshwa na watu! Huonekana jeuri, kiburi na wakorofi.
Sasa mkuu, unaleta misimamo yako kwenye ajira ya watu?

Hata me nna misimamo yangu ambayo siko tayari kucompromise hivyo niliamua kuachana na masuala ya ajira ili nibaki na uhuru wangu.

Hakuna mtu anamkataza kuwa na misimamo yake lakin je, anapoifanyia ni mahali sahihi?

Watu wamejenga reputation ya club for years, kisha we mtu mmoja uje uharibu image sababu ya unachokiita misimamo yako?

Nakumbuka yule Papis Demba Cisse akichezea Newcastle alikataa kuvaa jezi yenye udhamini ya kampuni ya vileo kwa misimamo ya kidini, wakamkubalia then siku kadhaa mbele waka release picha zake yuko club anapiga whisky, kwa aibu ilibidi avae jezi na ile logo.

Sasa huyu Ozil ana huo utakatifu anaojifanya kuuwekea misimamo yake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…