Machache kuhusu Community Shield
1-|. Michael Arteta


Katika siku 45 ameifunga Liverpool mara 2, kaifunga Manchester United mara 1, kaifunga Chelsea mara 1, na kaifunga Manchester City mara 1, amewaonea sana hawa wanaojiita top six
2-|. Ameonyesha kuwa habatishi kwenye approach yake katika hizi mechi kubwa, kuanzia kwenye upangaji wa kikosi, format ya mfumo na mbinu zake zilifanikiwa sana, kwenye mechi ya jana alijiandaa kujilinda kwanza, alimuheshimu sana mpinzani wake, na pindi alipoupata mpira timu iliondoka kwa kasi kwenda kwenye lango la mpinzani,
3-|. Aubameyang, Mechi zote kubwa huamuliwa kikubwa na wachezaji wakubwa, nafasi moja aliyoipata ilitosha kuwaadhibu Liverpool, alicheza kwa kujituma sana, tatizo pekee linalomsibu ni aina ya wachezaji anaocheza nao, hawajui wasimame wapi au wakimbie katika nafasi zipi, walimfanya Aubameyang akose machaguo mengi ya kufanya pindi anapokuwa na mpira kwenye nusu ya adui
4-|. Mohamed Elneny, unaweza kumuita Maestro, alipokea akatoa na akauomba tena mpira, ni kiungo aliyekuwa active muda wote, alikaba, aliziba njia na aliondoka na timu kwenda kushambulia, uwezo wake wa kumiliki mpira na kutoa pasi nyingi za usahihi ziliifanya idara ya kiungo ya Liverpool kulazimika kutumia nguvu kubwa kuwapora mipira Arsenal
5-|. David Luiz, Mechi ya jana alitulia sana, aliupanga vyema ukuta wake na hakukubali kufanya makosa, timu yenye Salah, Mane na Firmino ni ngumu sana kuweza kuizuia lakini chini ya Luiz alionyesha inawezekana kama ukiwa na beki kiongozi kama yeye, usiku wa jana unaweza kusema Arsenal haihitaji tena beki
6-|. Martinez,


Ametusahaulisha kama yeye ni golikipa namba mbili, utulivu wake na uhodari wake wa kuzuia mipira usiguse zile nyavu ulimfanya Sadio Mane kuonekana kama Yikpe aliyenyoa, natamani niendelee kumuona kwenye mechi nyingi zaidi
7-|. Jurgen Kloop, Aliposhindwa kuiamua mechi kwenye kikosi cha kwanza kilichoanza alihitaji kuimaliza kwa kutumia wachezaji wa akiba, kibaya wajumbe walimpitisha lakini kamati kuu ikamkata,
8-|. Naby Keita, Ana vitu vingi vitamu na vinavyovutia katika miguu yake lakini hana pumzi, alipoingia alileta uhai na ubunifu mkubwa kwenye kiungo cha Liverpool, alipiga pasi nyingi sana zinazofika, aliiendesha timu na timu ikacheza kupitia yeye lakini dakika 10 za mwisho akawa amekata upepo, timu ikashindwa kwenda mbele, plan za Kloop alizoingia nazo zikafia kwenye miguu yake
9-|. Takumi Minamino, sina shida na goli alilofunga, shida yangu ni kutaka kuendelea kumuona akiaminiwa na kuanza kwenye kikosi cha kwanza, mjanja mjanja hivi halafu kama mguu wake una sumaku, alipoingia alikuja na maswali mengi kwa Hector Bellerin na Bellerin alipokosa majibu Arteta aliamua kumpumzisha
10-|. Sub ya Firmino, mpaka sasa sijui kwanini alitolewa, sikuona kama Firmino alichoka wala sikumuona Firmino akiwa nje ya mchezo, wakati ambao Keita ameishiwa pumzi ndiyo wakati ambao Firmino alitolewa, ubunifu ukafa, akakosekana mchezaji aliyepandisha timu, akakosekana mchezaji ambaye angeamua timu ipitie wapi, wakati ambao Arsenal wakihitaji kupewa presha kubwa ndio wakati ambao walitulia na kuwapa presha Liverpool
----------------------------------
David Luiz alisema aliondoka Chelsea na kujiunga na Arsenal ili ashinde makombe, wengi walimpuuza lakini sasa hivi kashabeba mawili, baada ya kushinda kombe la Community Shield katika usiku wa jana, alisikika akisema yamebaki makombe mawili, kombe la Uefa Champions league pamoja na kombe la ligi kuu England, navyowajuwa mtasema tumpeleke Milembe

