Nishawekeana na mtu elfu mbili kwamba PSG hatoboi. Na wewe kama unataka weka.
Hahaha nazingua. Unajua PSG ana advantage ya kua na Neymar, Mbape, Di Maria na Icardi hawa wote wako vizuri hivyo kusema Bayern atashinda inataka moyo mgumu kidogo.
Lakini hoja yangu mimi naiegemeza kwa kuangalia game ya PSG na Atalanta na PSG na RB.
Atalanta alipiga pasi zaidi ya 350. RB alipiga pasi zaidi ya 415. Na wote walimshambulia sana PSG Navas alithibitisha ubora wake kwenye game na Atalanta.
Game na RB ilikua wazi kwamba RB wanachokosa ni striker. Poulsen hana kiwango cha kutisha uwepo wa Werner ungeisaidia RB siku wamekutana na PSG.
Bayern ameifunga Barcelona goli nane lakini alipiga pasi chini ya 414. Alivyocheza na Lyon alipiga pasi zaidi ya 450. Hii inamaanisha kwa Bayern ukijichanganya kumiliki mpira na kumshambulia kwa kujiamini yeye pasi zake zitakua ni za kutafuta mabao tu, wakati ukipaki basi atapiga pasi nyingi ili kupata chansi.
Now tujiulize, PSG atapaki basi? Naamini jibu ni Hapana. Huko kufunguka ndiyo kutaipa chansi Bayern kupiga pasi za kutafuta kuscore tu.
Ila nipo serious. Nimewekeana na mtu elfu mbili.