Wakati mwingine dunia huwa sio fair kabisa, yaani yule goigoi Ozil anachukua £350,000/= kwa wiki then Auba anabembeleza alipwe £250,000/= kwa wiki bado club inasua sua, na hatupo Uefa ila jamaa anatuvumilia, Auba akiondoka hatuna cha kumlaumu hata kidogo.
Hivi vimishahara mbuzi vinatufanya tupokonywe silaha zetu kila siku, Striker anaye contribute 30+ (goals + assists) kwa msimu tena kwenye timu mbovu kama yetu, akienda timu iliyokamilika ni balaa tupu.
Tukimpoteza Auba kupata striker wa kiwango chake labda tumuombee Martinelli awe na hiyo consistence, otherwise hatuna jeuri ya kumpata sokoni.