@Castr naomba nichangie na Mimi kidogo
Toka amekuja Arteta , Eneo la beki limeimarika ,hasa sababu tumekuwa na mfumo unaoeleweka ,kilichobaki ni kukosa ile Quality ya mchezaji,
Mfano beki za pembeni Yule Kieran Tierny ,ni Quality player kuanzia commitment, n.k bado pia Saka ni backup nzuri huu upande
Upande wa kulia bellerin kashuka sana , sababu nadhan ni ile ACL , Cedric sio mbaya wanapeana challenge na belle ,
Mabeki wa kati ndipo panahitajika ongezeko ,
Mustafi amekuwa msaada toka aje Arteta ,hata holding ameimarika tena baada ya kutoka majeruhi ya ACL ambayo wachezaj wengi huwa hawarud kwenye viwango vyao vya awali.
Luiz ,kola,sokratis hawa ndio wamekuwa na matatizo ya kutoku concentrate na mchezo, mech na Spurz ,kosa la Kola ndio limesababisha kufungwa ,
Ujio wa Saliba na ongezeko la beki mmoja litasaidia sana
Maana tutakuwa na Angalau Quality ya kutosha eneo la beki, huku luiz akitumika muda mchache
Nije eneo la kiungo , Xhaka ndio muhimili wa timu ,huyu piga ua tunauhitaji sana , ndiye atakayeungana na viungo wajao ,kina Partey ,n.k
Toreira aliharibiwa na Unai, alipokuja Arteta ,alihitaji kiungo wa kucheza na Xhaka awe na uwezo wa kupiga pass mbele ,sio wa kudefend zaidi
Ndio maana Ceballos akapata nafas zaid hata kabla Toreira hajaumia ,lakini unapohitaji mech za kukaba sana mwanzo mwisho ,toreira ndio kaz zake ,rejea mech ya Liverpool juzi,
Ceballos hana uzoefu sana, lakini ni aina ya kiungo mzuri sana , sema Arteta anamtumia sana chini ,juu anamuweka Xhaka,Ceballos anatumika kama DLP(Deep lying playmaker)
Awe anafanya clearance , kudefend na kupiga forward passes mbele ,na hii kaz kaiweza
Shida inakuja kwa aina ya soka la Xhaka , sio mnyumbulifu ,ndio maana tunamis ufund wa kina Nasri, carzola , Uncle Tommy,Hleb
Xhaka anajua kupiga Range pass tu,
Ndio sababu Bodi inamuhitaji Partey, Roca au Dominic
Kwahiyo shida kubwa eneo la kiungo hatuna ubunifu, ndio maana viungo wetu uchangiaji wao wa magoli ni mdogo sana
Arteta anajiandaa kutumia 4-3-3
Hapo tutapata uchangiaji mkubwa wa magoli kutoka viungo .