Watu wa JF wanajulikana si tu kwa username bali pia kwa michango yao na aina yao ya uandishi, mfano leo hii
milangomitatu watu wq humu tunamjua hata akija na account 10 na tunaishi nae so kwa uandishi huu wewe unaonekana ni mgeni humu pia upeo wako inaonesha kabisa ni u20 so upo kwa foolish age,
Kwanini hamjifunzi kukaa kimya?mfano Mimi kuliko kuwavurugia watu amani na kujishushia heshima kama sina hoja ya msingi naamua kuwa mpenzi msomaji wa michango ya wengine na siku zinaenda,
Siri ya mafanikio ni kuwa na upendo pia kuishi vizuri na majirani zako,
Kama jambo huna uelewa nalo soma michango ya wengine ujifunze,
Na haka katabia kuna hizi account
ENZO ,
papaa G na
Gpili mnatakiwa sana mjifunze kuishi na watu vizuri, maana hata matusi kwenu ni kawaida tu,sasa humu JF watu wanatumia sana acc fake unaweza kuta
Aaron ndio mchungaji wako hapo kanisani kwenu ,
King Ngwaba ndio baba yako mzazi au wa kufikia na
Don Clericuzio ndio shemeji yako mume wa Dada yako ambaye amekununulia hiyo smartphone unayotumia kumtukana humu,
Elimu ya mitandao ya kijamii imewapitia kushoto sana .
Mwenye masikio na asikie