#Gooners!
ilikua mechi nzuri yenye amsha amsha, tumecheza vizuri kiasi na nyota wa mchezo kwa leo binafsi nampa Leno na Mustafi.
Walifanya vizuri sana kila mmoja kwa nafasi yake japo kua Leno alifanya uzembe goli la pili lakini alifanya saves nyingi zilizo tuweka mchezoni.
Arteta pia alikua spot on kwenye kufanya sub, alifanya defensive substitutions ili kukabiliana na hatari iliyokua ikiletwa na washambuliaji wa Everton.
Na kuhakikisha tunamaliza mechi kwa ushindi.
Mwanzo tulikua tunasumbuliwa na game management kuanzia kwenye kulinda ushindi tukiongoza na kuhakikisha tunapata point tatu.
Muda mwingine haijalishi umezipataje hizo point tatu, na kiukweli point za leo zina umuhimu sana kwa sisi kuisaka top 5.
Tatizo nililoliona leo ni udhaifu kwenye set pieces, magoli yote tuliofungwa na kukoswa koswa yametokana na set pieces.
Nadhani Mari akipata match fitness tutatatua hili suala.
Pia Hector anaonekana bado hana match fitness na alionewa sana na Richarlison, nadhani kadri Muda unavyo kwenda atakua sawa.
Lacazatte hajacheza ila nadhani kuna umuhimu wa yeye kuanza match ijayo, presence yake ndani ya uwanja huleta faida nyingi hasa hasa kwenye zile link up play.
Hata hivyo Nketiah kajitahidi na nimeelewa kocha anajaribu kufanya kitu gani.
Timu ilionyesha uchovu na ni kawaida ikiwa umecheza michezo 3 ndani ya siku 7...Nategemea hali itakua tofauti mechi ijayo.
Nawapongeza pia kwakua kwenye mechi tatu hizi wachezaji wamejituma na kushinda mechi zote.
Alama chini ya 10 wachezaji wote nawapa 7/10....ila kwa Leno na Mustafi ni 7.5.