Richard
Platinum Member
- Oct 23, 2006
- 16,636
- 25,617
ORNSTEIN | Mauricio Pochetino ndiye chaguo la kwanza la Arsenal kama mrithi wa Unai, kinacho subiriwa ni jibu lake tu.
Changamoto za kumpata Pochetino ni 2 ambazo ni ndogo sana na zina tatulika yaki tengenezwa mazingira mazuri:
1. Alisha weka wazi kwamba hatokuja kuwa kocha wa Arsenal kutokana na uhasimu wetu na Spurs.
2. Malipo ya £12m ya Kipengele cha kuvunja mkataba na spurs endapo asipo ajiriwa tena ndani ya miezi 6.
#coyg![]()
![]()
Mkuu, Chaguo namba moja la Arsenal ni Brendan Rogers
Leicester wamesema watataka 14M za fidia ambazo Raul na Edua hawataona shida kwani watamweleza mzee Kroenke na familia yake.
Huyu anazungumza kiingereza safi na anawasiliana uzuri na kwa usahihi na media..
Media presence ya Arsenal imeporomoka sana hivi karibuni hivyo wanataka ku-fix hiyo.
Wakimchukua Rogers basi Leicester inashuka chini na Arsenal itapanda juu.
Hivyo Freddie ataipeleka timu hadi msimu uishe na huenda wakamchukua Rogers kabla ya msimu ujao ila itategemea na matokeo ya sasa ya Freddie.
Kwa uifupi wanataka Arsena ileile ya Arsene Wenger yaani mawasiliano mazuri na media na kiingereza.
Pochetino na Allegry ni chaguo jingine ila ni kwa sababu hizohizo za hapo juu, Arsenal wanaona Rogers anafaa zaidi kwa malengo ya muda mrefu.
Nuno ni chaguo namba mbili lakini nae ana rekodi nzuri tu kutokana na Wolves lakini bado hajanyakua kombe lolote.
Kuna Marcelino aliekuwa Valencia ambae ae ndo kwanza sasa hivi anajifunza hii lugha ya kiingereza, lugha ya wala mayai.
Hivyo tusubiri mazee Raul Sanllehi na Edu watakapoanza mchakato kuwapigia simu walengwa wote Jumatatu.
Idea ni kuirudisha Arsenal kukekule ilikokuwa kwenye mpira wa mashambulizi mengi na mgoli kwa wingi.
