Freddie Ljumberg.
Wengi wamefurahishwa kuchaguliwa kwa Ljumberg kuwa kocha wa muda wa arsenal. Kufurahishwa kwao kunatokana na sababu kuu tatu hiv;
1. Aliwahi kuichezea arsenal kwa mafanikio makubwa huku akiwa sehemu ya kile kikosi kilichochukua kombe bila kufungwa. Hivyo wengi wanaona Ljumberg ataleta ile hari ya ushindi iliyokuwa kwenye timu aliyocheza.
2. Good communicator and very charismatic. Moja ya changamoto kubwa aliyokuwa nayo Unai ktk klabu ya arsenal ni mawasiliano hafifu haswa kwa kuwa hakujua lugha ya kiingereza vizuri. Mara nyingi iliripotiwa kuwa wachezaji walikuwa hawaelew maelekezo wanayopewa kwasababu ya lugha gongana. Na hii ndio sababu iliyopelekea Ljumberg kupandishwa kutoka under-23 hadi kuwa kocha msaidizi. Ljumberg anasifiwa kuwa ni mcheshi pia na mtu ambaye huongea na wachezaji vizuri. Na ndio maana wengi wanaamini atasaidia kuiboresha timu.
3. Uwezo wake wa kufundisha soka zuri la kushambulia na kuongeza ubora wa wachezaji. Ljumberg alijizolewa sifa katika klabu ya arsenal kutokana na uwezo wake wa kufundisha soka zuri na kuboresha viwango vya wachezaji wakati akiwa anafundisha arsenal under-23. Huko inasemekana alifundisha soka safi la pasi za kutoka nyuma hadi kwenda kufunga huku akiboresha viwango vya wachezaji kama willock, Saka, Burton, john-jules, trae coyle, Arthur okonkwo, smith-rowe na wengineo. Katika msimu wake wa kwanza na under-23 aliiwezesha kushika nafasi ya pili. Hivyo wengi wanaona kuwa ljumberg anaweza kufanya alichofanya under-23 katika timu ya wakubwa.
Changamoto atakazokuna nazo ni;
1. Kukosa uzoefu mkubwa. Ljumberg hana uzoefu mkubwa katika nafasi ya ukocha haswa akiwa kocha mkuu. Nakumbuka nafasi ya kwanza ya ukocha kumsikia Ljumberg akiwa nayo ni pale alipokuwa anafundisha arsenal under-15, baadae akaongozana na aliyekuwa director wa academy ya arsenal Andres jonker kwenda kufundisha timu moja kule ujerumani ambako hawakudumu baada ya kutimuliwa. Baadae ndio akarudi under-23. Hii ndio changamoto kubwa kwake.
Maoni yangu ni kwamba sitarajii mambo makubwa kutoka kwa kocha huyu ila naamini kabisaa kiwango cha soka cha arsenal kitaboreka na arsenal itaanza kucheza mpira wa kuonekana
View attachment 1276935