Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Pre-season tour and league matches 2018/2019
837d31841ace867da10828d11f10b5a1.jpg
 
Arsenal wakamilisha usajili wa Sokratis Papastathopoulos kutoka Borussia Dortmund.

kama ilivyokuwa ikitarajiwa Arsenal jana walikamilisha usajili wa mchezaji huyo ambae amesaini mkataba wa miaka mitatu.


gettyimages-989807398-e1530613957845.jpg


Sokratis anakuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa na Arsenal baada ya beki mwingine
Stephan Lichsteiner na kipa Bernd Leno.

gettyimages-989815914.jpg


Sokratis anaungana na beki Calum Chambers ambae wiki ilopita alisaini mkataba wa muda mrefu na wataziba nafasi za Per Mertesacker aliestaafu na Laurent Koscielny ambae ni majeruhi na anatarajiwa kurudi uwanjani mwakani.

Per Mertesacker anakuwa meneja wa kitalu au shule ya vijana kwa jina la Arsenal Academy.
 
Usajili Updates: Arsenal kukamilisha usajili wa kiungo Lucas Torreira hivi karibuni.

gettyimages-988387724.jpg

Lucas Torreira.

Arsenal hivi karibuni wanatarajiwa kukamilisha usajili wa mchezaji kiungo mkabaji Lucas Torreira baada ya fainali za kombe la Dunia kufikia tamati.

Mchezaji huyo wa kiungo wa Samprodia ya Italy anatarajiwa kusaini mkataba utaogharimu kiasi cha pauni milioni 26.

Kwa sasa Torreira anajiandaa pamoja na timu yake ya taifa ya Uruguay kucheza na Ufaransa siku ya Ijumaa kwenye hatua ya robo fainali za kombe la dunia.
 
Arsenal wafanya mazoezi mafupimafupi

gettyimages-990671540.jpg

Unai Emery akiwa uwanjani London Colney tayari kuanza mpango wake wa mazoezi.
gettyimages-990723802.jpg

Emery amemleta kocha wa magolikipa aitwae Javi Garcia ambae pichani anazungumza na kipa namba moja wa Arsenal Petr Cech.

gettyimages-990723196.jpg

Emery akiwa na kocha msaidizi Steve Bould ambe amebakizwa baada ya kuondolewa jopo la wasaidizi wa Arsene Wenger.
gettyimages-990723768.jpg

Beki mshahara mpya Sokratis Papastathopolous akiwa mazoezini.
 
Usajili Updates: Arsenal kukamilisha usajili wa kiungo Lucas Torreira hivi karibuni.

gettyimages-988387724.jpg

Lucas Torreira.


Arsenal hivi karibuni wanatarajiwa kukamilisha usajili wa mchezaji kiungo mkabaji Lucas Torreira baada ya fainali za kombe la Dunia kufikia tamati.

Mchezaji huyo wa kiungo wa Samprodia ya Italy anatarajiwa kusaini mkataba utaogharimu kiasi cha pauni milioni 26.

Kwa sasa Torreira anajiandaa pamoja na timu yake ya taifa ya Uruguay kucheza na Ufaransa siku ya Ijumaa kwenye hatua ya robo fainali za kombe la dunia.
Huyu lazima tumpate---
 
Back
Top Bottom