Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Lichtsteiner was at Colney holding talks with [HASHTAG]#AFC[/HASHTAG] earlier today. Deal is not done yet and the next few hours will be decisive.


Mkuu Huyu Jamaa si Ana Umri Wa Miaka 34 Kweli Anaweza Kuwafaa au Ataishia Kuvizia Bellerin aumie ili na Yeye Acheze?
 
Mkuu Huyu Jamaa si Ana Umri Wa Miaka 34 Kweli Anaweza Kuwafaa au Ataishia Kuvizia Bellerin aumie ili na Yeye Acheze?

gettyimages-960206282.jpg

Stephan Lichtsteiner akiwa kazini

Bellerin alikuwa hana msaidizi baada ya kuondoka kwa Debuchy hivyo huyu Lichtsteiner ambae ni beki mzoefu anasajiliwa bila ada yaani free agent na atakuwa beki wa kulia wa akiba.

Beki mshahara Lichtsteiner ameisaidia Juventus kunyakuwa makombe 14 tangu mwaka 2011 na sasa amechoka kucheza Serie A.

Ilikuwa aende Uchina lakini ameamua aingine pale London ajikusanyie pesa ya kustaafu.

Arsenal pia wanataka kusajili beki mpya wa kushoto kuchukua nafasi ya Nacho Monreal mwenye umri wa miaka 32 ambae huenda akamaliza msimu ujao.

Hiyo ni kwasababu Saed Kolasinac ndiye atakaechukua nafasi ya Monreal lakini kutahitajika beki wa ziada, kumbuka kila nafasi ina wachezaji wawili.

Jina la Mbrazil Kenedy beki wa kushoto wa Chelsea anaechezea Newcastle kwa mkopo linazungumzwa.

Kenedy

Kenedy mwenye umri wa miaka 22 nae alishindwa kucheza pale Chelsea kutokana na kuwepo kwa Marcos Alonso na ndiyo maana akapelekwa Newcastle kwa mkopo.

Kenedy ni mmoja wa wachezaji waloisaidia sana Newcastle kubakia kwenye ligi kuu ya Uingereza.
 
Meneja mpya wa Arsenal Unai Emery amesema anataka klabu hiyo kuwa miongoni mwa klabu bora zaidi Ulaya kwa mara nyingine, na hata bora duniani.
Alisema hayo alipohutubiwa wanahabari kwa mara ya kwanza baada ya kuteuliwa kuwa mrithi wa Arsene Wenger.
Mkufunzi huyo wa miaka 46 aliwasilishwa rasmi kwa mashabiki na wanahabari Jumatano kabla yake, akiandamana na afisa mkuu mtendaji Ivan Gazidis kuhutubia waandishi wa habari waliokuwa wamefika kwa wingi.
Alisema: "Ufanisi msimu ujao utakuwa bado tunaukuza, lakini kwa jinsi gani? Kwa kupigania kila taji.
"Hilo limo ndani ya historia ya Arsenal na yangu mwenyewe."
 
Arsenal wana nia ya kumleta kiungo wa kati wa Roma Lorenzo Pellegrini huko Emirates. Muitalia huyo wa miaka 21 pia analengwa na Juventus. (Sky Sports)
 
Arsenal wana nia ya kumleta kiungo wa kati wa Roma Lorenzo Pellegrini huko Emirates. Muitalia huyo wa miaka 21 pia analengwa na Juventus. (Sky Sports)

Yupo pia kiungo Jean-Michael Seri wa Nice mwenye umri wa miaka 26.
c81db976-3d65-4b0b-b25f-a8882e11484a.jpg

Seri anatoka Ivory Coast.

Mwezi January mwaka huu Emery akiwa PSG alijaribu kumsajili Seri lakini akaambiwa zinatakiwa kama Euro milioni 29 hivi.
 
Mkuu Huyu Jamaa si Ana Umri Wa Miaka 34 Kweli Anaweza Kuwafaa au Ataishia Kuvizia Bellerin aumie ili na Yeye Acheze?
yah huyu anakuja kuleta changamoto tu ukuzingatia jamaa ni mzoefu pia atamfanya dogo apumzike maana kuna baadhi ya mechi kama zile za kombe la ligi na FA jamaa atasaidia sana kwani bado ana kiwango kizuri umri namba tukwani milner ana miaka mingapi sasa hivi na anaupiga mwingi tu.....yaya toure,young wote ni 30's na wapo fiti
 
yah huyu anakuja kuleta changamoto tu ukuzingatia jamaa ni mzoefu pia atamfanya dogo apumzike maana kuna baadhi ya mechi kama zile za kombe la ligi na FA jamaa atasaidia sana kwani bado ana kiwango kizuri umri namba tukwani milner ana miaka mingapi sasa hivi na anaupiga mwingi tu.....yaya toure,young wote ni 30's na wapo fiti


OK Powa Sana
 
Yani nyie uyo cocha enu hatamaliza msimu.

Mapema tu mtaanza mlilia wenga.

Subiri, taimu will teli.
 
Usajili Arsenal News!


Sokratis Papastathopoulos.

Kama nilivyodokeza huko juu post namba 59625, Arsenal wapo karibu kukamilisha usajili wa beki wa kati wa kimataifa wa Borusia Dortmund na timu ya taifa ya Ugiriki Sokratis Papastathopoulos.

Mkuu mpya wa idara ya usajili na ukuzaji vipaji wa Arsenal bwana Sven Mislintat ambae aliwahi kushika nafasi hiyo kwenye timu hiyo ya Dortmund , anataka kuhakikisha kwamba Sokratis anasajiliwa na Arsenal kwa namna yoyote ile kuimarisha safu ya ulinzi wa timu hiyo.

Sokratis Papastathopoulos anatarajiwa kusajiliwa kwa kitita cha pauni za Uingereza milioni 13.

Sokratis amechezea Dortmund kwa miaka mitano na kabla ya hapo alichezea timu ingine ya Ujerumani ya Werder Bremen.

Kabla ya kucheza Bundesliga Sokratis alicheza mpira nchini Italia kwenye timu za Genoa na AC Milan.

Sokratis amechezea nchi yake ya Ugiriki mara 79 hususan kwenye michuano ya Fainali za mataifa ya Ulaya ya mwaka 2012 na fainali za kombe la Dunia mwaka 2014.

Mkoba huyu ana uzoefu wa kutosha kabisa kushiriki kuiimarisha safu ya ulinzi ya Arsenal ambayo msimu ulopita wa 2017/2018 yameingia magoli zaidi ya 22.

Sokratis atakuwa mwalimu wa beki mwingine mkoba ambae ni mdogo Konstantinos Mavropanos, mwenye umri wa miaka 20 na ni mgiriki pia.

Lakini pia Sokratis anakuja kuziba nafasi ya "Boss" na nahodha Laurent Koscienly ambae ameumia.
 
Usajili Arsenal News!


Sokratis Papastathopoulos.

Kama nilivyodokeza huko juu post namba 59625, Arsenal wapo karibu kukamilisha usajili wa beki wa kati wa kimataifa wa Borusia Dortmund na timu ya taifa ya Ugiriki Sokratis Papastathopoulos.

Mkuu mpya wa idara ya usajili na ukuzaji vipaji wa Arsenal bwana Sven Mislintat ambae aliwahi kushika nafasi hiyo kwenye timu hiyo ya Dortmund , anataka kuhakikisha kwamba Sokratis anasajiliwa na Arsenal kwa namna yoyote ile kuimarisha safu ya ulinzi wa timu hiyo.

Sokratis Papastathopoulos anatarajiwa kusajiliwa kwa kitita cha pauni za Uingereza milioni 13.

Sokratis amechezea Dortmund kwa miaka mitano na kabla ya hapo alichezea timu ingine ya Ujerumani ya Werder Bremen.

Kabla ya kucheza Bundesliga Sokratis alicheza mpira nchini Italia kwenye timu za Genoa na AC Milan.

Sokratis amechezea nchi yake ya Ugiriki mara 79 hususan kwenye michuano ya Fainali za mataifa ya Ulaya ya mwaka 2012 na fainali za kombe la Dunia mwaka 2014.

Mkoba huyu ana uzoefu wa kutosha kabisa kushiriki kuiimarisha safu ya ulinzi ya Arsenal ambayo msimu ulopita wa 2017/2018 yameingia magoli zaidi ya 22.

Sokratis atakuwa mwalimu wa beki mwingine mkoba ambae ni mdogo Konstantinos Mavropanos, mwenye umri wa miaka 20 na ni mgiriki pia.

Lakini pia Sokratis anakuja kuziba nafasi ya "Boss" na nahodha Laurent Koscienly ambae ameumia.
Halafu wamuuze Shkodran!!!
 
- The Washington Post
Ujinga wa nchi za Kiafrika ndo huu. Yaani nchi masikini kama Rwanda inaweza kugenerate $13M kila mwaka kuilipa timu ya Wazungu wakati vitu kama Umeme, Maji ya kuaminika, vitendea kazi shuleni na mahospitalini hakuna. Hata kama mimi ni mpenzi wa soka la Arsenal siwezi kukubaliana na ujinga kama huu. Muda si mrefu utashitukia hata sisi Tanzania tunaiga upuuzi huu.
Btw, hivi Kikwete aliwalipa kiasi gani Premier League sijui Sunderland tulipokuwa tunaiadvertise misimu miwili sijui mitatu iliyopita?
Cc. Nzi, Belo, DonDonald, Malafyale, RRONDO etc
 
- The Washington Post
Ujinga wa nchi za Kiafrika ndo huu. Yaani nchi masikini kama Rwanda inaweza kugenerate $13M kila mwaka kuilipa timu ya Wazungu wakati vitu kama Umeme, Maji ya kuaminika, vitendea kazi shuleni na mahospitalini hakuna. Hata kama mimi ni mpenzi wa soka la Arsenal siwezi kukubaliana na ujinga kama huu. Muda si mrefu utashitukia hata sisi Tanzania tunaiga upuuzi huu.
Btw, hivi Kikwete aliwalipa kiasi gani Premier League sijui Sunderland tulipokuwa tunaiadvertise misimu miwili sijui mitatu iliyopita?
Cc. Nzi, Belo, DonDonald, Malafyale, RRONDO etc
Aisee no comment,sijasomea marketing.
 
- The Washington Post
Ujinga wa nchi za Kiafrika ndo huu. Yaani nchi masikini kama Rwanda inaweza kugenerate $13M kila mwaka kuilipa timu ya Wazungu wakati vitu kama Umeme, Maji ya kuaminika, vitendea kazi shuleni na mahospitalini hakuna. Hata kama mimi ni mpenzi wa soka la Arsenal siwezi kukubaliana na ujinga kama huu. Muda si mrefu utashitukia hata sisi Tanzania tunaiga upuuzi huu.
Btw, hivi Kikwete aliwalipa kiasi gani Premier League sijui Sunderland tulipokuwa tunaiadvertise misimu miwili sijui mitatu iliyopita?
Cc. Nzi, Belo, DonDonald, Malafyale, RRONDO etc
Marekani walipoanzisha USAID, au JAICA JAPAN hawakujua kuwa kuna masikini nchini mwao. Ni suala la mikakati, je hiyo return yake ikoje? Itajenga shule ngapi, maji yataenea kiasi gani kutokana na sponsorship hiyo.?
 
- The Washington Post
Ujinga wa nchi za Kiafrika ndo huu. Yaani nchi masikini kama Rwanda inaweza kugenerate $13M kila mwaka kuilipa timu ya Wazungu wakati vitu kama Umeme, Maji ya kuaminika, vitendea kazi shuleni na mahospitalini hakuna. Hata kama mimi ni mpenzi wa soka la Arsenal siwezi kukubaliana na ujinga kama huu. Muda si mrefu utashitukia hata sisi Tanzania tunaiga upuuzi huu.
Btw, hivi Kikwete aliwalipa kiasi gani Premier League sijui Sunderland tulipokuwa tunaiadvertise misimu miwili sijui mitatu iliyopita?
Cc. Nzi, Belo, DonDonald, Malafyale, RRONDO etc
Imesikitisha wengi, tuna uhakika ni ubabe tu Kagame umefanya yawezekane, kweli viongozi afrika ni majanga..
 
Back
Top Bottom