Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Wenger bonge la kocha, tatizo Kroenke anayesema vilabu vyake sio kwa ajili ya makombe. Kumuuzia yule Mrusi hataki, Wenger yulee Psg, au Everton kwa waarabu
 
Tetesi

Klabu ya Chelsea inapewa kipaumbele cha kunasa saini ya mlinzi wa Napoli, raia wa Senegal Kalidou Koulibaly mwenye umri wa miaka 26 anayewaniwa pia na klabu ya Arsenal na Manchester.

Arsenal,Leicester na Southampton wanafikiria kumsajili Mohamed Elyounoussi wa Basel.Mshambuliaji huyo, 23, raia wa Norway alifunga goli dhidi ya Manchester City katika ligi ya mabingwa siku ya Jumatano.
Wenger amsajili Yedder yule wa kuifunga Man U ,hasira zote za wapenzi zitaisha
 
Our opponents (last 8)
IMG_4595.JPG

Draw itakua kuanzia saa 8 mchana.
 
The Europa League quarter-final draw will be made at 12:00 GMT (07:00 ET) on Friday, March 16.
The first leg of the quarter-final ties will take place on Thursday, April 5, with the reverse fixtures to be played a week later on Thursday April 12.
 
ARSENAL imeanza kumfukuzia kinda wa Kibrazili, Maycon, anayekipiga katika klabu ya Corinthians ya Brazil na inadaiwa kuwa klabu yake ipo tayari kuachana naye kwa dau la Pauni 9 milioni tu.

Kiungo huyo alikuwa anakaribia kujiunga na Shaktar Donetsk katika dirisha la Januari, lakini uhamisho huo ulikwama na sasa Arsenal imekuwa mstari wa mbele katika mbio za kumsaka katika dirisha kubwa la majira ya joto.
 
RAIS wa Real Madrid, Florentino Perez inadaiwa anataka kumnasa beki wa kulia wa Arsenal, Hector Bellerin, kwa ajili ya kumpa changamoto Dani Carvajal ambaye hana mpinzani katika nafasi hiyo.

Inadaiwa Arsenal ipo tayari kuachana na beki huyo katika dirisha kubwa lijalo la majira ya joto endapo kuna timu itafika dau la Euro 50 milioni, lakini Madrid pia inaweza kukumbana na upinzani kutoka Juventus.
 
Danny Welbeck alifunga mabao mawili Alhamisi na kuwawezesha Arsenal kuwalaza miamba wa Italia AC Milan 3-1 na kufuzu kwa robofainali katika ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League.
Mshambuliaji huyo alitamba kwenye siku ambayo aliitwa tena kwenye kikosi cha taifa cha Uingereza.
Arsenal walikuwa wakiongoza 2-0 kutokana na matokeo ya mechi ya kwanza San Siro lakini walijipata taabani pale Hakan Calhanoglu alipofunga akiwa hatua 30 kutoka kwenye goli baada ya kuwazidi ujanja wakabaji wa Arsenal.
Arsenal walisawazisha upesi, ingawa kupitia mkwaju wa penalti uliogubikwa na utata, baada ya Welbeck kuanguka alipoguswa kidogo na mchezaji Ricardo Rodriguez eneo la hatari.
Alifunga mkwaju huo.

Na baada ya kipa maarufu wa Milan Gianluigi Donnarumma kubwagwa na kombora la mbali la Granit Xhaka, Welbeck alifunga bao la tatu kupitia mpira wa kichwa.
Ushindi huo uliwawezesha Arsenal kufika robofainali katika michuano mikuu ya klabu Ulaya kwa mara ya kwanza tangu 2010.
Watafahamu watakutana na nani robofainali droo itakapofanywa Ijumaa saa 12:00 GMT.

Ikizingatiwa kwamba Arsenal wamo alama 12 kutoka eneo la kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya katika Ligi ya Premia, ushindi Europa League inaonekana kuwa njia yao pekee kwa sasa kwao kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu ujao.

Ili kutimiza hilo, watahitaji mabao kutoka kwa Welbeck, ikizingatiwa mchezaji wao waliyemnunua Januari Pierre-Emerick Aubameyang haruhusiwi kucheza msimu huu kwani alishawachezea Borussia Dortmund.

Nini kitafuata?
Arsenal watapumzika wiki mbili kabla ya kurejea dhidi ya Stoke City Ligi ya Premia uwanjani Emirates mnamo 1 April (13:30 GMT).
AC Milan watarudi kusaka ushindi wao wa tano mtawalia wa ligi ya Serie A watakapokuwa wenyeji wa Chievo Jumapili (14:00 GMT).
 
Menaja wa Arsenal Arsene Wenger amesema angependa sana Arsenal wasipangwe kukutana na Atletico Madrid ya Uhispania katika ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League.
Hii ni baada ya Gunners kulaza AC Milan ya Italia 3-1 (Jumla 5-1) katika hatua ya 16 bora.
Atletico Madrid wamekuwa wakicheza vizuri na walifika robofainali Europa League baada ya kuwalaza Lokomotiv Moscow 5-1 mechi ya marudiano.
Nyota wa zamani wa Liverpool na Chelsea Fernando Torres alifunga mabao mawili nao Angel Correa, Saul Niguez na Antoine Griezmann wakafunga moja kila mmoja Alhamisi na kuwawezesha Atletico kupata ushindi wa jumla wa 8-1.

Atletico wameshinda Europa League mara mbili na walifika fainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mara mbili 2014 na 2016 - walishindwa mara zote mbili.
Mabao ya Arsenal yalifungwa na Danny Welbeck (mawili) na Granit Xhaka naye Hakan Calhanoglu akawafungia Milan bao la kufutia machozi Alhamisi.
"Bila shaka tungependa kuwakwepa Atletico Madrid," alisema Wenger.
Hata hivyo, alisema hana usemi wowote na wakikabidhiwa klabu hiyo hawatakuwa na budi ila kukutana nao.

Droo ya robofainali - ambapo kuna klabu nane kutoka mataifa manane - itafanyika leo Ijumaa saa 12:00 GMT.
Huu ulikuwa ushindi wa tatu wa Arsenal katika kipindi cha wiki moja baada ya kuwalaza Milan 2-0 mechi ya kwanza mjini Milan na pia wakalza Watford 3-0 Ligi ya Premia Jumapili.
Lakini kabla ya ushindi huo San Siro, walikuwa wameshindwa mechi nne mtawalia mashindano yote - mara mbili ikiwa mikononi mwa Manchester City.
"Mambo ni mazuri sana leo. Tulihitaji kujikwamua kutoka kwa matokeo yetu," Wenger alisema.
"Inaonesha jinsi timu ilivyochukua hatua. Tulikuwa na mechi ngumu lakini mwishowe tulishinda. Tukiwa na matokeo mazuri na jinsi tunavyocheza soka, mashabiki watatuunga mkono."

Ilikuwa mechi wazi. Tulicheza kwa kurejesha mpira nyuma mara nyingi zaidi kipindi cha kwanza kujilinda na kujaribu kutetea matokeo ya mechi ya kwanza. Tulicheza dhidi ya timu nzuri sana," alisema Wenger.
"Ni lazima tujiimarishe katika safu ya ulinzi, lakini kwa jumla yetu ni timu yenye ustadi kiufundi ambayo zaidi huangazia kushambulia.
"Huwa twatatizika zaidi wakati tunahitajika kujilinda. Tulimaliza mechi hiyo tukiwa imara zaidi."

Bao alilofunga Welbeck kupitia mkwaju wa penalti lilizua utata kwani Welbeck alionekana kuguswa tu kidogo kabla ya kuanguka na mwamuzi kuwapa Arsenal penalti.
Wenger alisema angetoa jibu baada ya kutazama tena tukio hilo

Lakini meneja wa AC Milan Gennaro Gattuso alisisitiza kwamba haikufaa kuwa penalti.
"Kwa njia sawa ambapo mchezaji anaweza kufanya kosa, mwamuzi anaweza kufanya kosa," alisema.
"Hata mimi mwenyewe nilipokuwa mchezaji, ningejaribu kufaidi kutokana na nafasi kama hizo. Sitatoa hukumu kuhusu hilo."
Kiungo wa kati wa zamani wa England Jermaine Jenas aliambia BT Sport kwamba ni wazi Welbeck alijiangusha.
"Hilo linatia kasoro matokeo hayo kidogo. Ni Wenger mwenyewe aliyesema kwamba wachezaji wa England wameanza kuzidi katika kujiangusha; ilikuwa ni mmoja wa wachezaji wake leo."
Ushindi huo uliwawezesha Arsenal kufika robofainali katika michuano mikuu ya klabu Ulaya kwa mara ya kwanza tangu 2010.
Wakati huo waliondolewa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya na Barcelona kwa matokeo ya jumla ya 6-3.
Ikizingatiwa kwamba Arsenal wamo alama 12 kutoka eneo la kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya katika Ligi ya Premia, ushindi Europa League inaonekana kuwa njia yao pekee kwa sasa kwao kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu ujao.
 
Cska moscow hawez kutusumbua, naona mpinzani wetu hasa ni atletico, vijana wa el cholo, wengine waliobaki hawatupwelepweti.
 
Back
Top Bottom