Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Naona ile thread ya "nimeacha rasmi kuishabikia Arsenal" itakosa wachangiaji kwa muda. Ni pamoja na zile hashtags maarufu.
 
IMG-20180309-WA0010.jpg
 
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger alifananisha klabu yake na bondia ambaye anajikakamua kuinuka baada ya kupigwa kondena kuangushwa ulingoni na jinsi klabu hiyo ilivyojikwamua na kulaza AC Milan 2-0 katika Europa League baada ya msururu wa matokeo mabaya.
Wenger alisema pia kwamba matatizo hayadumu.
Arsenal walikuwa wanakabiliwa na uwezekano wa kushindwa mara ya tano mtawalia wka mara ya kwanza tangu 1977 walipoandikisha ushindi huo wa kuvutia uwanjani San Siro.

Mabao kutoka kwa Henrikh Mkhitaryan - aliyetawazwa mchezaji bora wa mechi - na Aaron Ramsey yaliwaweka vijana hao wa Wenger katika nafasi nzuri ya kufika robo fainali katika ligi hiyo ndogo ya klabu Ulaya.

Ni ushindi muhimu sana kwa sababu tulikuwa na wiki ya masaibu," alisema Wenger.
Gunners walikuwa wamecharazwa na Brighton katika Ligi ya Premia Jumapili, baada ya kulazwa mara mbili mfululizo 3-0 na Manchester City katika fainali ya Kombe la Ligi uwanjani Wembley na katika Ligi ya Premia.
Aidha, walikuwa wamelazwa pia 2-1 na wanyonge wa Sweden Ostersunds FK, ambapo walinusurika kutokana na ushindi wao mkubwa mechi ya kwanza na kusonga hadi hatua ya 16 bora ambapo walipangwa kucheza na Milan.

Mashabiki wa klabu hiyo wameendelea kumshutumu Wenger, huku asilimia 88 ya wanachama wa Wakfu wa Mashabiki wa Arsenal (AST) ambao una wanachama wakipiga kura mapema wiki hii kuunga mkono mkataba wa Mfaransa huyo mwenye miaka 68 utamatishwe mwisho wa msimu.
Hii ina maana kwamba Arsenal walifika San Siro uungwaji mkono wa Wenger ukiwa chini sana katika miaka 22 ambayo ameongoza klabu hiyo.

Lakini walicheza kwa ustadi mkubwa saa na kuwaonjesha Wataliano kichapo cha kwanza kabisa katika mechi 13.
"Unapokuwa na masikitiko makubwa huwa unasahau upesi kwamba una sifa fulani nzuri. Katika kipindi cha wiki moja, haugeuki na kuwa timu baya au mchezaji mbaya. Hakuna linalodumu milele maishani," amesema Wenger.

Unapoangushwa inakuwa kidogo ni kama katika mchezo wa masumbwi ambapo unakuwa umeangushwa na mchezaji chini, hauna muda wa kutosha wa kuinuka na kujikwamua na unapokezwa konde jingine. Hilo lilitutendekea.
"Lakini inafika wakati fulani ambapo unajua ni lazima uchukue hatua. Sifa zako na hamu yako ya kutaka kuonyesha ustadi ni lazima vionekane katika mchezo."
 
Tetesi

Klabu ya Chelsea inapewa kipaumbele cha kunasa saini ya mlinzi wa Napoli, raia wa Senegal Kalidou Koulibaly mwenye umri wa miaka 26 anayewaniwa pia na klabu ya Arsenal na Manchester.

Arsenal,Leicester na Southampton wanafikiria kumsajili Mohamed Elyounoussi wa Basel.Mshambuliaji huyo, 23, raia wa Norway alifunga goli dhidi ya Manchester City katika ligi ya mabingwa siku ya Jumatano.
 
Tetesi

Beki kisiki wa Arsenal Hector Bellerin, 22, anakaribia kujiunga na Juventus ya nchini Italia. (Bleacher Report, via Mirror)

Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 26 amesema hajakaribia kusaini mkataba mpya huku mkataba wake wa sasa unafikia mwisho ndani ya muda wa miezi mitatu ijayo. (Independent)
 
Tetesi

Beki kisiki wa Arsenal Hector Bellerin, 22, anakaribia kujiunga na Juventus ya nchini Italia. (Bleacher Report, via Mirror)

Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 26 amesema hajakaribia kusaini mkataba mpya huku mkataba wake wa sasa unafikia mwisho ndani ya muda wa miezi mitatu ijayo. (Independent)
Wilshere ni mmoja wa mediocre players at arsenal that are overrated just because of his nationality. He should explore other venues now.
 
HT
Arsenal 1-0 WAT
Kipindi cha pili kusipokua na mabadiliko basi itakua ngumu kupata alama 3 leo maana kule mbele sioni kama kuna mipango ya kueleweka.
 
Back
Top Bottom