Numbisa
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 348,112
- 1,249,107
Matokeo ya mechi yatategeme jinsi Manchester United wanavyocheza katika mechi hii ya Emirates
Jose Mourinho amekuwa na tabia ya kupaki basi kwenye mechi kubwa za ugenini, jambo linaloashiria mechi hii inaweza kuishia sare.
Licha ya hilo, ni vigumu kuona jinsi mechi hii itakavyomalizika bila magoli.
Moja ya mahasimu wakuu wa Ligi ya Uingereza watakwaana Jumamosi Arsenal watakapoikaribisha Manchester United katika uwanja wa Emirates.
Manchester United walishinda 4-2 dhidi ya Watford Jumanne usiku. Timu ya Mourinho wakienda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 3-0 shukrani kwa Anthony Martial na mabao mawili kutoka kwa Ashley Young.
Mabao ya kipindi cha pili kutoka kwa Troy Deeney na Abdoulaye Doucoure yaliipatia United utisho kabla ya Jesse Lingard kufunga goli la nne.
Arsenal wameshinda mechi saba Ligi Kuu Uingereza katika uwanja wao wa nyumbani msimu huu (kama walivyofanya Manchester United).
United wamepoteza mechi tatu kati ya tano za mwisho kwenye michuano yote ugenini.
Mbinu ya Mourinho kucheza kwa kujihami kumeifanya United kuondoka bila goli mechi za ugenini Liverpool na Chelsea.
Arsenal hawajaruhusu goli katika mechi zote sita ambazo Laurent Koscielny, Shkodran Mustafi na Nacho Monreal walianza kwa pamoja kwenye safu ya mabeki.
Jose Mourinho amekuwa na tabia ya kupaki basi kwenye mechi kubwa za ugenini, jambo linaloashiria mechi hii inaweza kuishia sare.
Licha ya hilo, ni vigumu kuona jinsi mechi hii itakavyomalizika bila magoli.
Moja ya mahasimu wakuu wa Ligi ya Uingereza watakwaana Jumamosi Arsenal watakapoikaribisha Manchester United katika uwanja wa Emirates.
Manchester United walishinda 4-2 dhidi ya Watford Jumanne usiku. Timu ya Mourinho wakienda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 3-0 shukrani kwa Anthony Martial na mabao mawili kutoka kwa Ashley Young.
Mabao ya kipindi cha pili kutoka kwa Troy Deeney na Abdoulaye Doucoure yaliipatia United utisho kabla ya Jesse Lingard kufunga goli la nne.
Arsenal wameshinda mechi saba Ligi Kuu Uingereza katika uwanja wao wa nyumbani msimu huu (kama walivyofanya Manchester United).
United wamepoteza mechi tatu kati ya tano za mwisho kwenye michuano yote ugenini.
Mbinu ya Mourinho kucheza kwa kujihami kumeifanya United kuondoka bila goli mechi za ugenini Liverpool na Chelsea.
Arsenal hawajaruhusu goli katika mechi zote sita ambazo Laurent Koscielny, Shkodran Mustafi na Nacho Monreal walianza kwa pamoja kwenye safu ya mabeki.

