Arsenal waanza kuondoa wachezaji wasumbufu.
Chamberlain anafanya mazungumzo ya kujiunga na Chelsea, timu zimekubaliana ada ya uhamisho pauni milioni 35.
Timu ya Chelsea mchana huu imekubaliana na Arsenal kumsajili moja wa wachezaji muhimu Alex Oxlade Chamberlain na kiasi cha ada ya uhamisho kinasemwa ni pauni milioni 35.
Alex Oxlade Chamberlain hivi sasa yupo kwenye kambi ya timu ya taifa ya Uingereza.
Meneja wa Chelsea Antonio Conte anakata kumtumia Ox kucheza kwenye nafasi ya beki wa kulia ambayo Chamberlain huicheza anapokuwa Arsenal kiasi ca kuitwa "most versatility player" yaani anaweza kutumika kucheza nafasi mbalimbali.
Ox Chamberlain wiki ilopita alifanya mazungumzo na Arsenal juu ya mkataba mpya ambapo aliwekewa mezani kiasi cha pauni 180,000 kwa wiki kaisi ambachi alikataa.
Chelsea inatarajia kumlipa Ox kiasi cha pauni 200,000 kwa wiki.
Arsenal ipo katika mtihani mgumu msimu huu baada ya jana jumapili kufungwa goli alba yaani 4-0 na Liverpool huko Merseyside ambapo wachezaji Fimimho, Mohamed Salah, Sadio Mane na Daniel Sturridge walifunga goli hizo alba.
Arsenal haikuonyesha kabisa kujituma katika mchezo huo na mshambuliaji Alex Lazazette ambae alisajiliwa kwa kiasi cha pauni milioni 60 alianzia kwenye orodha ya wachezaji wa akiba.