Usajili Updates: Arsenal wanaidhoovisha Leicester, huenda wakamsajili Riyad Mahrez pia.
Wakati Arsenal wakiwa wanangojea Jamie Vardy akamilishe taratibu za kusajiliwa, huenda wakamsajili pia Riyad Mahrez ambae ni mshambuliaji mwenza wa pembeni wa Jamie Vardy.
Klabu ya Leicester katika kujaribu kumzuia Vardy asiende Arsenal jana usiku waliweka dau kubwa Zaidi kwa mshambuliaji huyo lakini tayari ilionekana amekwishafanya Medical na yupo tayari kutia saini karatasi muhimu.
Pia wakti huohuo jana jioni Arsenal walidokezwa kwamba mkataba wa Riyad Mahrez haukuwa umeshiba vya kutoha hivyo kuanza utaratibu waharaka wa kuomba kufanya mazungumzo na mchezaji huyo wa Leicester.
Mahrez alijiunga na Leicester Januari mwaka 2014 akitokea timu ya Le Havre ya France kwa gharama ya pauni 400,000.
Mwezi August mwaka jana Leicester waliboresha mkataba wa Mahrez lakini haijulikani una gharama ya kiasi gani ambapo inakisiwa kuwa swa na ule wa Jamie Vardy ambapo kuna kifungu kilichowekwa kinachosema kwamba:-
"Endapo timu ingine kubwa inayocheza kwenye "champions league", itajitokeza kutaka kufanya mazungumzo ya usajili, basi timu hiyo itatakiwa kulipa gharama ya pauni milioni 20."
Hivyo kwa mara ingine tena Arsene Wenger ameamuru wataalam wake waanze kazi na waimalize kabla au baada ya Euro 2016.
Arsene Wenger alikwishafanya utafiti na mtandao wake wa maskauti ukiongozwa na Gilles Grimandi nchini Ufaransa kwa Mahrez, lakini akaghairi na kuja kushtushwa na uchezaji wa Mahrez akiwa Leicester City.
Ikiwa mambo haya yatakuja kuwa fully confirmed basi Arsenal watakuwa wamefanya biashara moja maridadi sana.
Tusubiri baadae kidogokwa habari zaidi.
Stay Tuned.