Team news,
Arsenal kesho inacheza na Chelsea uwanja wa Emirates ikiwa ni mechi ya tatu msimu huu.
Mechi ya kwanza ilikuwa ni ile ya Community Shield ambapo Arsenal ilishinda kwa goli 1-0.
Mechi ya pili Chelsea walishinda kwao kwa goli 2-0. Katika mechio hii Gabriel alitolewa kwa kadi nyekundu baada ya vituko vya Diego Costa na baadae Santi Cazorla nae katolewa kwa kadi ya pili ya njano.
Hivyo basi Arsenal kesho inatarajiwa kuonyesha kwamba imezonga mbele kimpira na wapo tayari kukabiliana na timu yoyote ile.
Ikumbukwe kwamba Arsena ina mechi karibu sita za ugenini dhidi ya Man Utd, Everton, Tottenham, West Ham na kukaribia mwisho wa ligi dhidi ya Man City.
Habari nzuri ni kwamba majeruhi wamerudi na Mesut Ozil na Alexis Sanchez watacheza kesho.
Mesut bila shaka ataanza mechi hiyo na Sanchez huenda akaanzia bench maana haitakuwa vema kuanza moja kwa moja kutokana na kuogopa kutonesha musuli.
Fransic Coquelin na Thomas Rosicky wamepona na wameanza mazoezi magumu, Danny Welbeck anaanza mazoezi wiki ijayo na Jack Wilshere anatarajiwa kuanza kucheza tena mwishoni mwa mwezi February.
Kiungo mpya Mohamed Elneny huenda nae akaanzia bench.
Hivyo basi timu inayotarajiwa kuingia uwanjani kupambana na the blues ni kama ifuatavyo:
Kipa Petr Cech, beki kulia Bellerin, kushoto nacho Monreal.
Mabeki wa kati ni Mertesacker na Boss.
Mlinzi wa kati ni Mathieu Flamini au Mohamed Elneny.
Kiungo wa kati ni Aaron Ramsey na mbele yake Mesut Ozil.
Washambuliaji wa pembeni kulia ni Joel Campbell na kushoto ni Theo Walcott.
Mshambuliaji ni Olivier Giroud.
Haya basi tukutane kesho jioni kabisa tayari kushuhudia miamba ikiumana.