Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Ramsey anamvuta Silva kwa nyuma na anapewa kadi ya njano na mwauzi Andre Marina.

Timu bado zinasomana mbinu na hakuna anaeanza mashambulizi ya dhati.

Dakika inakwenda ya 11
 
Arsenal wao wanacheza na mtindo wao wa 4-3-2-1.

Man City wanaonekana wanacheza mtindo wa 4-1-4-1 huku Fernandinho na David Silva wakijaribu mashuti ya mbali.
 
Dakika inakwenda ya 14 na inahisiwa kwamba kna mpango wa kutoa sare.

Ila simwamini Yaya Toure anajifanya hachezi kihivyo, lakini akipata mpira ndani ya eneo la Arsenal anakuwa amepata uhai mpya.
 
Arsenal wanafanya makosa kuwaachia Man City wamiliki mpira kwa kiasi kikubwa.

Hii nafikiri ni hatari sana hasa ukiwa unacheza nyumbani.
 
De Bruyneeeee no Petr Cech analala na kukamata mpira.

Ni shuti la kwanza kwa Man City.

Dakika inakwenda ya 26
 
Kuna jambo lingine la kuvutia, kila mara Olivier Giroud anapopata mpira basi anazungukwa na mabeki kama watatu hivi wa Man City, hii ni heshima kubwa.

Dakika inakwenda ya 28
 
Arsenal na Man City wameanza kucheza mpira sasa.

David Silva nae anapewa kadi ya njano na mwamuzi Marriner.

Dakika inakwenda ya 30 na goli ni 0-0
 
Bakary Sagna akiwa amesimamishwa kwenda mbele na Theo Walcott ambae akapata nafasi ya kuingia ndani ya eneo la hatari na kuachia shuti kali ambalo kipa Joe Hurt hakuwa na nafasi ya kuzuia.

Goli limefungwa dakika ya 33

Arsenal 1 Man City 0
 
Hii ni ajabu sana kuona Arsenal wanawaruhusu Man City kumiliki sehemu kubwa ya mpira huku wao Arsenal wakiweza kufanya mashambulizi ya kushtukiza na kufunga.

Otamendi nae anamchezea vibaya Oliveir Giroud.

Giroud yupo fit na anaendelea na game.

Dakika inakwenda ya 42

Arsenal 1 Man City 0
 
Mesut Mustapha Macho Ozil haachi kuassist niamini mimi
 
Mesut Ozil ndie amesababisha magoli yote mawili kweli anastahiki dau la milioni 42

What a creative midfielder!
 
Back
Top Bottom