Naomi bwana mdogo Sanogo kakamilisha usajili wa mkopo pale crystal palace mpaka sasa hakuna ingizo jipya pale emarate.
mkuu
Richard vipi tetesi zinasemaje kama zipo zitupie hapa jamvini.
Mkuu,mambo vipi?
Kama nilivyokwishasema hapo kabla kwaba huyu Yaya Sanogo na Lucas Podolki walikuwa waondolewe kwenda kwenye mkopo.
Podolski huenda asirudi kuchezea Arsenal tena kutokana na kauli anazozitoa wakti huu akiwa kule Italy kwamba meneja Wenger alipenda kumuacha bench.
Yaya Sanogo amekwenda Crystal Palace kwa mkopo na hio ni ishara kwamba atarudi Arsenal akiwa na uzoefu wa PL na umakini katika umaliziaji.
Sasa suala la usajili ni kwamba mpaka sasa kuna mchezaji mmoja ambae huenda akatangazwa siku chache zijazo nae ni bwana mdogo kutoka timu ya Legia Warsaw aitwae Krystian Bielik ambae ni mchezaji wa kiungo na ana miaka 17.
Huyu dogo ana kipaji twaweza kumuita "Progidy" na anachezea Legia kwenye irst 11 yao. Alisajiliwa na Legia kutoka timu ingine ya Lech Poznan kwa kiasi cha paundi 9,500 akini Legia Warsaw wamewaambia Arsenal wakohoe kiasi cha paundi milioni 2.4 au Euro milioni 3 hivi.
Maskauti wa Arenal na wenzao wa Barani ulaya waitwao Scouting Polska na wengine wa FourFourTwo wanamwona kijana huyu akiwa na uchezaji mzuri huko siku za mbele hasa pale Mikael Arteta na Mathieu Flamini watakapomwaga manyanga baadae mwaka huu.
Kijana huyu ana uefu wa futi 6 na nchi 2 na ana umbo kubwa la kufanya aweze kucheza kama DM au CM au CD n alikuwepo London Colney (kambi ya Arsenal) mwezi wote wa December mwaka jana.
Pia kuna kijana mwingine aitwe Ilkay Gundogan wa Borrusia Dortmund ya Germany ambae amekataa kusaini mkataba na timu yake hiyo.
Inasemwa kwamba Dortmund wapo tayari kufanya dili la paundi 15 milioni.
Kwa kawaida usajili kwenye mwezi wa January huwa unakuwa mgumu kwasababu kila timu inakuwa na wasiwasi wa kupoteza mchezaji muhimu hivyo kuweka dau kubwa kama ambavyo tunaona Man City wanavyofanya kwa Wilfried Bony.
Si kwamba Arsenal wanashindwa kutumia milioni 30 kufanya usajili lakini ni pale penye ulazima tu na ndio maana kunakuwa na kusita kidogo.
Hivyo tusubiri ntashuka tena baadae kidogo.