Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Dawa ilobaki ni kwa Arsenal kupakia basi kama zinavofanya timu zingine zinapokuwa na watu 10.

Ila Bayern nao wana wachezaji wawili wenye kadi za njano ambao ni Jerome Boateng na Mario Mandzukic.

Arsenal kipindi cha pili watacheza mtindo wa 4-5-1 na Yaya Sanogo atakuwa mbele peke yake ingawa Olovier Giroud anaweza kuingia mwishoni mwa kipindi cha pili.

Bayern wao watakuwa wakimshughulisha Nacho Monreal na hasa Robben na Lahm ingawa Mario Gotze na Mandzukic watakuwa wakijaribu kupokea vyumba kutoka kwa Thiago au Kroos na hasa mipira mirefu.

Twaviamini vitasa viwili pale nyuma Mertesacker na Coscielny.
 
kiuhalisia...tumebakiza Substitution moja tu....nayo aingie Thomas Rosicky...na inalazimika tema iwe behind the ball...kwa nguvu zote...wakae deep ili kuwa frustrate bayern munchen...

Anko Tom ndo mtu pekee kwa game hii anaeweza leta changes
 
Kipindi cha pili kimeanza na Bayern wamefanya mabadiliko kwa kumtoa Jerome Boateng na nafasi yake kuchukuliwa na Rafinha.e

Ikumbukwe Boateng ana kadi ya njano.
 
Sasa mbona ya ozil haikuwa red card hii mipango cjui itaisha lini, lakini acha tuone

wakati OZIL anaangushwa kulikuwa na mabeki wengine wa bayern,Boateng hakuwa last man....lakini kipa wa arsenal alikuwa last man,ile ni clear goal scoring opportunity
 
Bayern wameamua Thomas Muller apashe misuli kujiandaa kuingia.
 
Mesut Ozil anaanza tena kuwa mvivu.

Anaachia mipira mingi iwaendee wachezaji wa pembeni wa Bayern na harudi nyuma ulinzi.a kusaidia safu y
 
sasa kipindi hiki cha pili ni kushambuliwa mwanzo mwisho.....all guns blazing...ooopsss
 
Back
Top Bottom