Thanks Gunner.
what a terrible game!
Nilisema mapema kuwa, kuwakosa Aaron Ramsey na Theo Walcott ni pigo kubwa sana kwetu kwa sababu hawa walikuwa mpaka wanamfanya hata Olivier Giroud aonekane ni mshambuaji hatari wakati kiuharisia ni average player ambaye hawezi hata kwenda na playing style ya Arsenal. Slow, dreadful first touch, immobile....
Kukaa hapa na kusema tungeshinda hii mechi wakati hatujashinda ni kujifariji faraja ambayo haina impact yoyote katika uharisia.
Gosh, Sijawahi kuona timu mbovu kutokea katika viunga vya mitaa ya Sir Matt Busby Way, Old Trafford kwa muda mrefu kama hii Man United ya mwaka huu lakini cha kushangaza ndiyo imeondoka kwenye viunga vyetu vya Emirates Stadium na point moja kibindoni kitu ambacho kwa Man United hii ni ushindi.
Ukiangalia na kuchunguza utagundua kuwa tulikuwa tunacheza mpira with fear of the unknown kama vile tunapambana na Man United ya Sir Alex Ferguson wakati wachezaji wa Man United pia walikuwa na wasiwasi mkubwa wa kufungwa as a result, Man United were excellent defending deep and in numbers,
Let's forget and move on kwa sababu kuna makombora Jumapili yako mbioni tena kushuka Emirates kutoka Merseyside saa 16:00 GMT kwa ajiri ya mtifuano wa FA CUP fifth round. Hata hivyo, nina uhakika hiyo mechi tutashinda.
Tukutane tena kwenye kijiwe chetu hiki Jumapili.
Once a Gunner, Always a Gunner.