Tofauti kubwa iliopo leo ni kati ya Christian Benteke na Olivier Giroud, wakti Benteke anashindwa kumiliki mipira ndani ya eneo la Arsenal, mwenzie Giroud anafanya hivyo na akapata goli la pili ndani ya sekunde 59.
Pia Mathieu Flamini kwa upande wa Arsenal amecheza vema na kuilinda vema back four ya Arsenal huku Jack Wilshere akiruhusiwa kwenda mbele na hata kufunga goli la kwanza.
Ozil nae amekuwa busy upande wa kushoto akisaidiana na Serge Gnabry ambae nae amejaribu kwavuruga mabeki wa Aston Villa.
Ila Santiago Cazorla hana siku nzuri leo na amekuwa akipoteza mipira mingi bila sababu na haitakuwa jambo la kushangaza kuona anatoka na nafasi yake kuchukuliwa na Thomas Rosicky.