Peasant
JF-Expert Member
- Sep 27, 2007
- 3,949
- 699
Taja watatu? alafu Henry huwezi kujivunia kuwa kaibuliwa na Arsenal. Tatizo lenu mnaanzia kufuatilia wachezaji wakishafika Arsenal.
kw hyo unataka kusema henry alkuwa star kabla ya kuja arsenal, naomba nipe vigezo mkuu...
Wewe mdwanzi kweli Henry amekuja arsenal akitoka Italy nadhani Juventus akiwa mchezaji wa kawaida na zaidi alikuwa anatumiwa kama winga, amekuja London akatengenezwa akawekwa kati akaanza kutupia kama hana akili nzuri, wewe ndio mshabiki oya oya ambae umeanza kufatilia EPL baada ya ABROMOVICH kuinunua CHELSEA.
Kumbe mpo wengi mlioanza kufuatilia mpira juzi, Henry alikuwa mkali toka akiwa Monaco (1992-1999). Soma vizuri habari zake utakuja kuthibitisha hilo na aliweka record nyingi tu ikiwepo kufunga magoli mengi kwenye UEFA (1997-1998) kuliko mchezaji mwingine mfaransa.
Suala la kutoka Juve akiwa wa kawaida ni suala la Ligi na mfumo wa Italy ulimkata pia unatakiwa kukumbuka kuwa hakukaa sana Juve, ametoka Monaco kwenda Juve January 1999 na Ameondoka Juve kwenda arsenal Mwaka huo huo mwezi wa nane.
Na kwa kujua kiwango chake hata bei yake ilikuwa juu pia arenal walimchukua kwa £11 million, Kwa miaka ya 1990s hiyo ilikuwa bei kubwa sana.
Acha hizo wewe ... Henry huko kote alikotoka alikuwa ni winger ..
Nani aliyemtengeneza akawa striker na finisher mzuri?
Jibu unalo hata kama hutaki kusema ?
Kwani alipokuwa Winga Monaco hakuwa anafunga?
Henry amekuja Arsenal akiwa ni world cup winner na ndio alikuwa mfungaji mwenye magoli mengi zaid kwa timu ya Ufaransa kwenye michuano hiyo ya mwaka 1998. Sidhani kama haujui mpira vizuri unaweza kuchaguliwa kwenye kikosi cha wakati huo cha Ufaransa kilichokuwa na vipaji kibao, achilia mbali kuwa mfungaji bora wa timu.