Wakuu mambo vipi.
Bantalanda, Rejao, Wacha, Kweli na wengine kuna mambo yanafanyika kuokomoa Arsenal.
Kuna habari jioni hii kwamba Tottenhama wamekuwa wakifanya usajili wa wachezaji wao hadi saba, huku wakati huohuo wakiwa wamezuia usajili wa Gareth Bale ucheleshwe kwa makusudi ili kuwazuia Arsenal wasimsajili Angel Di Maria ambae Arsenal walitaka wamsajili mapema wiki hii ili acheze Jumapili kwenye mechi ya Arsenal na Tottenham.
Bale amekwishakubali "terms" na Real Madrid na atatangazwa jumatatu baada ya mechi hiyo wa watani hao wa kaskazini mwa London.
Mwenyekiti wa Tottenham ambae ni mtaalam wa mbinu za usajili amemaliza masuala yote ya usajili wa Gareth Bale lakini amekubaliana na Real Madrid kwamba wakimruhusu Di maria azungumze na Arsenal mpaka mechi ya jumapili itakapochezwa.
Kumekuwa na taarifa mbalimbali kwamba kuna kampeni dhidi ya Wenger na Arsenal kuhakikisha kwamba hawapati wachezaji wa uhakika wanaowahitaji ambao watawaongezea nguvu katika timu mbayo ipo tayari kwenye ligi ya msimu huu.
Kuna baadhi ya vyombo vya habari ambavyo vilikuwa vikisubiri kwa hamu Arsenal ipoteze mechi kati yake na Fulham na Arsenal wakashinda ile mechi tena kwa ushindi mnono. Baada ya mechi ile hata yule msemaovyo Ian Wright akawa baridi kwa kiasi kikubwa katika mahojiano yake na televisheni na redio mbalimbali.
Baada ya mechi na Aston Villa vyombo mbalimbali vya habari vikiongozwa na moja ya televisheni maarufu nchini Uingereza, kwa makusudi kabisa viliweka kampeni ya kumharibia Arsene Wenger utaratibu wake wa kuandaa timu kwa ajili ya mechi na Fenerbahce na Fulham lakini Arsenal wakashinda mechi hizo.
Hivyo tusubiri Wenger atafanya nini ndani ya masaa 72 yaliyobaki, lakini usajili wa Angel Di Maria, Karim Benzema na Mesut Ozil unatarajiwa kukamilishwa baada ya Gareth Bale kutangazwa kuwa mchezaji wa Real Madrid siku ya jumatatu.
Tottenham mpaka kufikia jioni ya Ijumaa wamesajili wachezaji saba ambao wamegharimu kiasi cha paundi milioni 109, na kama wamefanya walichokifanya Queens Park Rangers basi tunasubiri.