Lucas podoski ni mchezaji mwenye jina kubwa na hasa kwa jinsi anavyofanya vizuri akiwa na timu yake ya taifa ya Ujerumani kwani anazaidi ya caps 100, kabla hata ya RVP kutuacha wenger alikuwa tayari ameshakamilisha deal la podoski na kumpatia namba 9 (naamini kwa namba 9 ile wenger alikuwa naandaa mazingira ya podoski kuwa mshambuliaji pale Arsenal na si winga wa kushoto)
Kama mnakumbuka game yake ya kwanza Arsenal alicheza kama striker dhidi ya FC cologne wakati wa majira ya kiangazi mwaka jana..ila baadae hakufanya vizuri sana pale kati (nafikiri wenger anamuona kwenye training sessions kuliko sie mpaka ilipoamuliwa anunuliwe mshabuliaji mwingine ambae ni Olivier Giroud, podolski hucheza kama striker iwapo tu giroud hayupo au mgonjwa..karibu na mwisho mwa msimu uliopita kwa mfumo wetu wa 4-2-3-1 wenger alimtumia sana Cazorla kushoto na giroud katikati au akianza kushoto ujue mechi haimalizi lazima atatolewa mpaka akapata "kisifa" cha kuwa mchezaji aliyefanyiwa sub kuliko yeyote kwenye EPL kwa msimu wa 2012-2013
Akipata nafasi anapiga magoli mazuri sana ila nafasi yake klabuni naiona ndogo sana, sasa najiuliza TATIZO la podolski ni nini??? Mi naona podo sio mchezaji wa kaliba ya Arsenal yaani haendani na mchezo wetu au mpaka kocha apate ufumbuzi amchezeshe kwenye nafasi gani na mfumo upi..kama mshambuliaji anakosa (movements kwenye box) kitu ambacho naona wenger keshakiona, kwenye winga ya kushoto anapiga mapande mazuri ila hana dribbling abilities na speed ya kuwaacha mabeki haraka..kwa kweli hawezi kuwapita mabeki kirahisi..huu ndio ukweli
Kwenye winga ya kushoto kwa wachezaji tulionao na mfumo tunaocheza santi na Alex oxlade chamberlain wanamzidi dribbling abilities na pace japo cazorla nae akiwa winga huwa anaingia sana kupitia kati tofauti na theo upande wa kulia ambae anapitia kwenye chaki…
Tunajua Gervas gervinho keshaondoka na upande wa kushoto yupo oxlade chamberlain (ambae kaumia) inawezekana anatafutwa natural left winger nah ii haitakuwa habari nzuri kwa podolski..sasa scouts hawakuwa makini na weakness na strength za huyu mchezaji??? (najiuliza)
Cha kushangaza Zaidi ni kuwa hata ujerumani pia mfumo wao ni 4-2-3-1 sasa kule anafanya vizuri huku tatizo nini????
Ebu tujadilini wadau…
Wacha 1
Viper MwafrikaHalisi Wandugu Masanja BAK Rejao Balantanda Oxlade-Chamberlain Richard