Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Kama nilivyosema hapo awali kwamba Blackburn wanacheza "10 behind tha ball" ndani ya eneo lao. Gervinho anawasumbua kwa sasa isipokuwa inabidi awe anaingia ndani ya eneo lao na washambuliaji wa Arsenal wanaweza kufunga.

Ila kuna dalili ya Arsenal kupata goli la kwanza.
 
Tunamiliki mchezo na Arsenal mpaka sasa wana kona 10 na kipa wa Rovers Jake Kean amepangua mpira wa kichwa uliopigwa na Abu Diaby na kukoa lililokuwa goli la Arsenal.

Blackburn hawaendi mbele na wapo happy kukaa na kulinda eneo lao.
 
Kona zote hiz no goal????

Tena Arsenal mpaka sasa wamepiga kona 11 na ya mwisho Vermaelen akapiga kichwa na kwenda pembeni ya nyavu.

Blackburn wanacheza kwa kujihami lakini wanashambuliwa na Arsenal.

Arsenal inabidi wawatumie vizuri wachezaji wa pembeni hasa Gervinho na Chamberlain ili waingie vizuri na mpira ndani ya 18 ili kupata goli.

Kwa sasa Giroud ndie anaekosa mipira mingi.

Kona ya 12 inakwenda sasa.

Halafu Gernivnho anachezeshwa upande wa kushoto maana anashindwa kutumia mguu wa kushoto kupiga mashuti. Inabidi ajaribu hivyohivyo.
 
Gervinhoooooo, anakosa goli la wazi kabisa na yeye anafahamu hilo. Ilikuwa ni move nzuri ya Rosicky na imepotea.
 
Halftime na ni 0-0

Arsenal walitakiwa wame na goli ambalo limepotezwa na Gervinho.


Arteta amekuwa akipika mashambulizi akisaidiwa na Diaby na Thomas Rosicky.
 
mbinu za ufungaji hakuna right wing tunatumia sana lakini tunashindwa na mbinu za kufunga
Blackburns wanajaribu kulinda sana ili kupata counter attack
 
Jamani coquelin le coq anatakata uzuri kweli beki 2!


Francis Coquelin ni versatile na anachezeshwa kama utility player kwamba anaweza kucheza namba yoyote na hii ni moja ya mafunzo ya mzee Wenger kwa wachezaji wa Arsenal.

Kwenye mechi na Sunderland unafahamu kwamba Bacary Sagna alicheza kama mkoba na akaimudu vema nafasi hiyo?

Coquelin anafahamu kuusoma mchezo na ana mbinu nzuri za kukabiliana na adui.
 
Francis Coquelin ni versatile na anachezeshwa kama utility player kwamba anaweza kucheza namba yoyote na hii ni moja ya mafunzo ya mzee Wenger kwa wachezaji wa Arsenal.

Kwenye mechi na Sunderland unafahamu kwamba Bacary Sagna alicheza kama mkoba na akaimudu vema nafasi hiyo?

Coquelin anafahamu kuusoma mchezo na ana mbinu nzuri za kukabiliana na adui.
Long live le coq!
 
Wakuu endeleeni kutupia Updates maana huku kwetu tunatumia Cable, hawaonyeshi mpira kwa leo. Vp Babu Wenger kamweka tena benchi L Podoski au la!
 
jamaa wanalinda ile mbaya
tunahitaji mashuti ya mbali najuwa sio mchezo wetu lakini sio rahisi kuupita ukuta wao
 
David Bentley anaingia kwa upande wa Blackburn na anapokewa kwa booos na wapenzi wa Arsenal.
 
Back
Top Bottom