Hello Gunners wenzangu mambo!
Hizi ni 3 points muhimu sana kuzingatia kwamba tukishinda mechi ijayo dhidi ya Aston Villa basi tutakuwa na picha kamili ya wapi tunasimama.
Mechi ya jana ilionyesha kwamba sasa timu yetu inaweza kusimama na kucheza mpira bila wasiwasi tena bila hata wachezaji wawili wa mkoba Vermaelen aleumia kiwiko cha mguu na Koscielny ambae aliumia kwenye mechi ya kirafiki na timu France.
Wenger hakuwa na jinsi na ikabidi amchezeshe Bakary Sagna kama mkoba na pembeni kulia kukawa na Carl Jenkinson na kushoto Monreal.
Kwa kweli hatukutarajia "line u"p ile lakini Sagna akacheza kama vile nafasi hiyo hucheza siku zote na takwimu zinaonyesha kamba aliokoa mipira mara 14, alikabili adui mara 1, aliingilia pasi 2, aliokoa mipira 5 ya vichwa, na alitoa pasi murua kwa asilimia 79.
Hii ni rekodi safi kabisa juu ya bakary Sagna ingawa uchezaji wake wa siku za hivi karibuni umeulizwa maswali mengi.
Everton wana game ngumu leo dhidi ya Man U ingawa wanaweza kuambulia sare.
Jana tulimpa mkono wa kwaheri Santos ambae anarudi kwao Brazil ambako anajiunga na timu ya Gremio kwa mkopo na pengine baadae uhamisho kabisa.
Halafu kuna mpango mzima wa Arsenal kufanya "clear out" ya wachezaji sita akiwemo Andrei Arshavin na Squillaci ambao mikataba yao inafikia tamamti mwezi Julai mwaka huu na wameambiwa kabisa watafute timu.
Jumamosi tarehe 16 tunawakaribisha Blackburn Rovers kwenye mzunguko wa tano wa kombe la FA na baadae Jummane tarehe 19 tunawakaribisha Bayern Munich ya Germany kwenye uwanja wetu wa Emirates.
Come on Gunners!